Monday, December 27, 2010

Jinsi ya kurembesha macho


UNAWEZA kuweka macho yako katika hali ya kupendezanakuhakikisha yanakuwa na mvuto wa kipekee.
Kama unataka kufanya macho yako yaonekane meusi pakawanja kulingana na aina ya macho yako bila kujali kama kamauna macho makubwa au madogo.
Kama una macho madogo unatakiwa kuchora mstari pembenibaada ya kupaka wanja, hii husaidia watu wenye machomadogo kuonekana kuwa wana macho makubwa.
Anzia kupaka kwenye kona za macho wakati mwingineunatakiwa kushikiria jicho wakati wa kupaka wanja.
Watu wenye macho makubwa wanashauriwa kupaka wanjawenye mistari myembamba ambayo inanakshiwa na urembo ndani yake.
Unatakiwa kuhakikisha kuwa, wanja unaotumia hauna madharakwa macho yako kwani kuna aina nyingine ya wanja mtuanapotumia macho huwasha au hutoa machozi.
Pia usipende kutumia kila aina ya wanja kwa ajili ya usalamawa macho yako, unaweza kutumia bidhaa za kampuni moja tu nasi kubadilibadili kila wakati.
Wakati wa kupaka wanja fuata mstari na rudi hivyo kwa marambili nyingine hadi kuhakikisha kuwa wanja umekolea vizuri.
Pia unaweza kutumia pamba kwa ajili ya kupaka shedo juu yamacho kwa rangi ambayo umechagua.
Hakikisha kuwa, unapokuwa unatengeneza macho yakounatakiwa ukae kwenye kioo na uwe umetulia ili kuwezakutengeneza macho yako vizuri huku ukitumia kioo ambacho kitakuonyesha vizuri.
Ni vizuri kuchagua tangi za kupaka na ni heri pia kama rangiunazochagua zinaendana na nguo au kiatu utakachovaa.Ni vizuri kupaka rangi ya kung'aa wakati wa usiku na pia rangizilizotulia wakati wa machana.
Unaweza kupaka mascara kwa kutumia brash kwa ajili ya kurembesha kope zako ili ziweze kuinuka na kuleta mvuto katika macho yako.

No comments:

Post a Comment