Tuesday, November 24, 2009

Pendezesha makalio yako kwa kufanya haya


Makalio yetu ndiyo yanayotoa shepu fulani kwa mwanamke katika vivazi na ukiyaachia ovyo yanaweza kukuletea mushkeli na kama ukiyatengeneza hata yale makalio yanayosifiwa sana.
Wanawake wengi kwa sasa wanapenda kurekebisha makalio yao ili kuyapatia ukubwa unaostahili kwa jinsi wao wanavyopenda.
Tatizo hili halipo hapa nchini lakini wapo walionitupia swali na sasa inabidi nikiri kuwa lipo sana Marekani na mpasuaji wa masuala ya urembo wa Miami Dk Constantino Mendieta amethibitisha.
Mtaalam huyu amezungumzia sana utunzaji wa makalio daraja la kwanza ndiyo yanayotakwa sana. Ni kama vile umeuchukua moyo halafu ukaugeuza chini juu,haya ndio dizaini ambayo Marekani wanalilia sana.
Watu wa huko wanajimwaga katika majumba ya upasuaji kupata shepu hiyo adimu, na anayewachengua sana.
Kama unataka kuwa na shepu bomba fuata hatua zifuatazo:
1. Fanya masaji na losheni zinazoimarisha na kutengeneza ngozi nyororo katika mapaja yako,ukianzia chini ya makalio mara mbili kwa siku.
2. Ondoa miinuko midogo midogo isiyotakiwa nyuma yako kwa kuskrabu mara mbili au tatu kwa wiki ukiwa na salt scrub.
3. Pamoja na matatizo ya michuchumio,ivae ili kukupata nafasi ya kutembea kwa miondoko ya twiga inayotoa nafasi nzuri kwa makalio kuwa na mvuto.
4. Tafuta namna nzuri ya kuficha michirizi ya kunyooka kwa misuli ya mwili.
5. Mazoezi yatakufanya uwe mtu tofauti zaidi, pandisha ngazi kwa dakika kumi au zaidi na kisha chukua mazoezi ya kubana makalio yako na sehemu ya kiuno kwa kusukuma kwa ndani na kutulia hivyo kwa sekunde tano na kujiachia na unaweza kufanya hivyo unavyotaka.
Pia unaweza kuongeza uzuri wa makalio yako kwa kuhakikisha kwamba unakula vyema na unakula lishe inayostahili.

No comments:

Post a Comment