Friday, May 20, 2011

Mikoba inavyochangia urembo wa mwanamke



UNAPOKUWA katika safari zako utaona jinsi wanawake wanavyobeba mikoba ya aina mbalimbali.
Wakati mwingine mingi ya mikoba huwachukiza na wengine huwa kichekesho na ingawa wengine urembo wao huambatanishwa na kujipachika tu, vitu maarufu kama vipima joto kwa lugha ya kileo.
Ukiangalia hasa mijini hakuna kabati la nguo la mwanamke ambalo litakosa mikoba, tena ya aina mbalimbali. Kwa mwanamke kuwa na mkoba moja si sawasawa, kwa wale wanaokwenda na wakati kuwa na aina nyingi ya mikoba hii hutokana na ukweli kuwa mikoba hiyo ni sehemu ya mavazi na huambatana na si tu aina ya pamba iliyopigwa bali aina ya viatu vinavyompa kampani mwanamke.
Mwanamke ni kiumbe mrembo kabisa na jinsi anavyozidi kumechisha vitu anatakiwa kuwa mrembo na mwangalifu zaidi kwani anahitaji kujiweka katika kiwango kinachostahili katika kazi zake na uonekano wake.
“Mavazi yako unayovaa yanaweza kabisa kubadili maisha yako” anasema Trinny Woodall mmoja ya watu ambao wako makini kabisa na masuala ya unadhifu wa wanawake wa wanawake katika mitoko ya aina mbalimbali aliyeko Afrika Kusini.
Inakuwaje unapokuwa na vazi tofauti na mkoba wako wa kwapani na ndiyo huo mkoba mmoja pekee unaotumia kwa kwenda pati, kwenda safari. Kwenda kazini na kadhalika?
Hakika kwa mwanamke anayejijali, anatakiwa kuwa na mikoba ya aina tofauti kwa kuzingatia haja ya shughuli zake na pia mavazi yake.
Unachotakiwa siku zote si tu kuwa na mikoba mingio, najua unaweza kuwa na mikoba, unaoupenda lakini ni dhahiri kwamba mikoba hiyo unatakiwa lakini ni dhahiri kwamba mikoba huyo inatakiwa kuwa na mwendo sawa na mavazi yako ili kukupa kitu bomba kinachoweza kuwafanya wanaume wakutazame mara mbili mbili na wanawake wenzako wakuonee gere.
Nina sababu ya kukuambia hivyo lakini wapo wanawake waliojaza mikoba kibao lakini hawaitumii lakini hapo mwanzao waliponunua walijua kwamba ni mikoba bomba kabisa yenye mvuto wa kimapenzi hasa.
Kitu cha kwanza kuzuia ni ule ufujaji wa kununua mabegi yasiyotakiwa, yaani ni kuwa makini na haja yako mwenyewe na mapenzi yako na namna wewe mwenyewe ulivyo.
Ndiyo kusema mkoba lazima uzinagatie mwili wako, upenzi wa maisha yako.
Watengeneza mikoba wengi wanaonya kabisa uchukuaji wa mikoba kwa kuiona bomba kumbe hairandani na wewe unayeibeba.
Mathalani wewe ni mrefu na mwembamba, mikoba yenye mduara ni mizuri lakini kama wewe ni mfupi uliyejazia kiasi chake mkoba unaofanana na ule wa mstatili, mrefu kiasi na mweroro ni kiboko yake.
Ningekushauri kabla hujanunua na kuvaa mikoba hiyo hebu jitazame kwanza katika kioo kwani ni lazima ukubali kwamba uko safi ndiyo uchangamke na mtaa, unapokuwa umejiangalia kwenye kioo utapata namna bora namna bora ya muonekano kama vile unavyojaribu nguo kwenye kioo.
Mikoba myembamba iliyobana hasa huonekana kuwa bomba kwao kama wewe ni mwembamba pia na kama unataka mtu kujisahau kwa namna yake katika mwili wako, lakini haitakusaidia sana kwa matiti yako ni madogo na mikono yako haijajaza inavyostahili.
Halafu tazama sana mikanda ya mikoba ina maana kubwa zaidi ni ndiyo maana ni vyema ikazingatiwa urefu wake katika mabega yako kwani kwa vyovyote vile urefu wake utakavyobeba mkoba wako ina kitu inakifanya katika mwisho wake.
Kwa hiyo kama hutaki mushkeri katika maeneo ya juu ya mapaja usitwae mkoba unaofika pale. Wengi wa wanawake hutokea bomba kama mkoba haufiki katika kiuno au juu yake kidogo, kwani kuketi hapo chini inakuwa mambo si poa katikati ya mwili kwa upande wa juu ndiyo haswaa sawa.
Ni muhimu ukitambua ya kwamba ukubwa wa mkoba wako unaambatana na wewe unaeleweka.
Lakini niseme moja tu mikoba mingi huwa bomba kama haijazwi vitu lakini mathalani kama una simu, shajara na vikorombwezo vya uzuri mkoba mwembamba haufai kwani utatuna na kuchukiza.
Mbunifu wa FUNEKA, Tasleem Bulbulia anasema kwamba mtu wa aina hii kwa kulingana na kazi zake na stahili zake za maisha mikoba mipana ni saizi yake. Ndiyo kusema kazi na stahili yako ndiyo pia itazingatia aina ya mkoba unaotakiwa kuwa nao.
Ulishatambua personaliti yako na aina yako ya maisha ni vyema ukatambua ukweli kuwa chagua kulingana na wewe na si yule kwani kivigezo haiwezekani na kwa maisha pia haiwezekani.
mwisho

Urembo wa macho utakufanya uonekane bomba zaidi


Eyeshadows ni urembo ambao hutumiwa juu na chini ya kope. Njia hii husaidia kuongeza kina na mwelekeo wa macho ya watu.
Watu wanapenda kutumia aina hii ya urembo ili kuweza kuimarisha muonekano wao.
Kama wewe ni mweusi jaribu kutumia rangi angavu ili kuimarisha muonekano wako ukitumia rangi za giza zitakufanya uonekane vibaya.
Ni muhimu kuhakikisha kuwa unakuwa makini ili kuweza kuweka macho yako katika hali bora zaidi ya kupendeza.
Wakati mwingine Eyeshadows hufanya macho kuonekana makubwa au madogo. Lakini cha muhimu kuzingatia je rangi unayopaka inaendana na macho yako au ngozi yako.
Unatakiwa kupaka rangi kwa ustadi mkubwa huku ukiweka mkolozo katika kona za macho yako.
Ni vizuri kama utatumia eyeshadow ya penseli kwani huwa rahisi kuitumia na inapatikana kwa urahisi madukani.Kuna rangi za aina nyingi ambazo hupendeza wapakaji, rangi hizo ni pamoja na pink plum, matumbawe na shaba, bluu na kijani
pamoja na fedha, dhahabu na nyingine nyingi.
Rangi hizi hutofautiana kulingana na mng'ao wake kwani kuwa zenye mng'ao mkubwa na zile zilizofifia.Njia ya kawaida ya kupaka eyeshadow ni kutoka ndani ya kona
ya jicho na nje na zaidi.Rangi kama Gray, violet, zambarau na bluu huwapendeza sana
watu wa rangi ya maji ya kunde na kusaidia kung'arisha macho yao.

Thursday, May 5, 2011

MZIO wa ngozi au aleji


MZIO wa ngozi au aleji ni tatizo linaloweza kukupata kutokana na mwili wako kukataa kitu fulani, hutokana na sababu ikiwemo hewa na hata chakula tunachokula.
Kimsingi ni matatizo ya mlipuko wa mfumo wa kuhami mwili kwa kutumia au kuwa katika eneo ambalo linatibua mfumo wa mwili kwa kitu ambacho pengine wengine wala hawana tatizo nacho.
Kuna vitu ambavyo huibua mzio kama vumbi katika nyumba, mavi ya panya, manyoya ya wanyama na hewa yenye aina ya spiriti.
Mzio unaweza kukufanya uwe na ukrutu, mafua, pumu na hata kuvimba kwa mwili.
Wapo watu ambao hupata tatizo la ngozi, kuwashwa na hata kujaa.
Kuna mambo mengi sana ya kujifunza, lakini inaonekana kuwa tatizo hili husababishwa na mazingira na wakati mwingine ni tatizo la kurithi.
Katika dunia ambayo inatamba sana na teknolojia, tatizo la mzio lipo kubwa na hasa kemikali zinazotumika katika vyakula na hata urembo vinapotibua kemikali zinazotengeneza aleji katika mwili.
Kuna dalili tofauti za kuelezea aleji (mzio), lakini ni kitu ambacho ama hakika kinaweza kutibua uzuri na urembo wako na hata wakati mwingine kufanya mtu usiwe na raha kwa kutokea ukurutu au kuvimba kwa mwili.
Kuna aleji mabaya kama za kuumwa na mdudu ambapo wengine hubadilika na kuvimba mwili au eneo na hata presha ya damu kupungua kabisa.
Pia kuna tatizo la kuwa na aleji na dawa na chakula.
Ninachotaka kukuambia kwa leo ni haja ya kuwa mwangalifu katika vitu vingi na mara nyingi inafaa mtu kuwa mtulivu na kuachana na kile kitu ambacho kinakuletea tabu.
Kama huna uhakika nini kinakuletea mushkeri, ni vyema kutafuta viashiria vyake kwa kumuona mtaalam wa aleji.
Sehemu kubwa ya aleji haitibiki, san asana wataalam watakupatia dawa Fulani za kukusaidia kupunguza makali, lakini kwa vyovyote vile hali hii unaweza kuimudu mwenyewe kwa kuhakikisha unaondokana na ulaji au utumiaji wa vipodozi vya ovyo ovyo.

Tai iendane na umbo lako


Kuna mambo mengi ya kufanya ili tuwe watu wa kuvutia kila wakati.Mpangilio wa mavazi hufanya mtu kuonekana maridadi.
Kama wewe ni mvaaji wa tai unapovaa unazingatia mambo yapi? Na je unafunga tai yako kwa namna inayokubalika?
Wengine huwa hawafahamu jinsi ya kufunga tai na hivyo kuleta mushkeri wakati wa kuvaa tai na kusababisha tai kukaa upande. Unapoamua kuvaa tai na shati ambalo halijanyooshwa ambalo linakuwa kwenye mikunjo au kuvaa tai na ndala unakuwa umeua maananzima na kulivunjia heshima vazi hili.
Tai ni vazi lawatu walio maridadi kama huwezi kuwa maridadi basi vazi hili halikufai kabisa.
Unapovaa taa unatakiwa kuzingatia aina ya umbo lako kama wewe ni mnene vaa tai inayoendana na mtu mnene na kama wewe ni mwembamba basi vaa tai inayoendana na mtu mwembamba.
Kuna wengine huvaa tai zinazofika magotini na kuwa kichekesho anapopita mtaani
Tai ni vazi ambalo huongeza heshima na hadhi ya mvaaji cha muhimu ni jinsi gani unavaa tai yako na ikiwezekana jaribu kumechisha tai na suruali kwa vile ili tai upendeze ni laima iendane na nguo unayovaa.
Ni vyema ukahakikisha kuwa unakuwa na tai zenye rangi tofauti ambazo zitaendana na nguo unazovaa.
mwisho

Tuesday, April 26, 2011

Jinsi ya kuwa bi harusi mrembo


KITU cha muhimu ni kuhakikisha unakuwa makini kwa kila unachokifanya hasa katika suala la kuweka mwili wako sawa.
Tabia ya kutaka kupunguza mwili kupita kiasi kwa kipindi kifupi inaweza kukuletea matatizo kiafya. Usijaribu kupunguza mwili katika kipindi cha miezi miwili kabla ya siku yenyewe ya harusi, kitu cha msingi ni kuanza kupanga mapema kupunguza uzito wako taratibu.
Ndiyo kusema kama unataka kuwa katika shepu unayoitaka wakati wa harusi yako basi jambo la kuzingatia ni kujiweka fiti.
Hatushtukizi harusi. Harusi zinapangwa kwa hiyo muda mwingine wa kuangalia unataka kutoka na shepu gani wakati wa harusi.
Pia usijaribu kupanga kitu kisichotekelezeka.
Wanawake wengi hutaka kujiweka katika umbile la kuwa wembamba zaidi ili kujaa katika gauni analotaka yaani kuwa kipotabo , kuwa mkweli kwako mwenyewe huwezi kuleta vurumai katika mwili wako ili tu uwe mwembamba, yaani usifikirie hata mara moja kwamba unaweza kujibadilisha unavyofikiria eti kwa kuwa unataka kuolewa.
Lakini la maana ni kuwa kama unataka kuonekana tofauti sana kiasi cha mwamba hata huyu mchumba asikutambue na marafiki wakushangae?
Kwa kawaida waolewaji huwa na muda mfupi sana na msululu wa mahitaji ili wapendeze, na kutokana na hili wengi wetu hujaribu njia za mkato nyingi zikiwa hazifai kujiweka katika mwili wa wembamba ambao tunadhani kuwa unapendeza.
Tafadhali usijaribu hata kidogo kuanza diet ambayo inatoa matokeo ya haraka huku ukiwa umetumia nguvu kidogo.
Pia achana na mpango wa kula vidonge vya kuzuia mlo au kula vidonge ambavyo vinakubana au kula aina moja ya supu kwa wiki nzima yaani ninachozungumzia ni achana na kubania mlo wako ukawa si ule wa kuleta virutubisho vyote.
Kuhusu vipodozi
Kuwa mwangalifu kuhakikisha kwamba hakuna kitu hakuna kitu kinachoharibu utaratibu wako wa kupendeza hasa ile rangi ya ngozi yako.
Usipende kutumia vitu vipya vikakututumua ukashindwa kuelewa hivi uso au mwili huu una matatizo gani? Kwani majaribuo humpeleka mtu katika balaa asilolijua.
La maana sana ni kutumia vipodozi maalum vya kulainisha na kuitonusha ngozi kwa jamu ili kuiwezesha kuwa na mafuta kiasi yanayoweza kutulia wakati wa kutengeneza vitu yaani make- up siku ya harusi, kitu ambacho mara nyingi pia husaidia ukiachia vipodozi hivyo maalum kuweka ngozi katika hali iliyotulia ni mazoezi, mara nyingi mazoezi huleta rangi maridhawa ya ngozi na kwa kuwa upo katika nchi yenye joto basi sehemu za wazi zifanywe zile mwanga wa kutosha kukamilisha rangi.

mambo ya beauty care


A Syrian hairdresser do makeup to a visitor during the "Beauty Care" exhibition at the Exhibition City of Damascus, Syria, on April 26, 2011. More than 140 Arab and foreign companies attended three exhibitions, "Beauty Care", "Furniture exhibition" and "Just Married", which kicked off simultaneously under the auspices of the Syrian Ministry of Economy and Commerce.

Thursday, March 3, 2011

'Singlet' kivazi kinachohitaji usafi zaidi


KUNA wanaume nawasifu kwa kuzingatia usafi wa mavazi yao na hata muonekano wao licha ya kuwa wengine wameamua kuliweka kando kidogo suala hili.
Unapokuwa mtanashati unakuwa na kila sababu ya kujiamini.
Usafi wa mwili umekuwa ukisisitizwa sana kutokana na ukweli kuwa usafi ni afya na muhimu kwa kila moja kuwa na tabia ya kuwa msafi wakati wote.
Usafi ni pamoja na kuoga na kutakata vizuri, kutorudia kuvaa nguo ambayo imevaliwa na inanuka jasho na hata kunyoosha nguo vizuri kabla ya kuvaliwa.
Singlet pamoja na kuvaliwa ndani ya shati pia zimekuwa zikivaliwa zaidi na wanamichezo ikiwemo mieleka na wale wa mbio ndefu.
Wengi wanavaa singlet ndani ya nguo nyingie iwe kwa wanaume au kwa wanawake
"Unaponunua singlet unazingatia zaidi ubora na kitambaa kilichotumika kutengeneza nguo hizo kama ni pamba au aina nyingine ya kitambaa, lakini wanaume wengi wanapendelea pamba zaidi" anasema mkazi mmoja wa Jijini Dar es salaam.
Uvaaji wa singlet unatakiwa kuzingatia zaidi usafi kutokana na ukweli kuwa nguo hiyo imekuwa ikivaliwa sana na wakati mwingine huathiriwa zaidi na jasho linalotoka mwilini.
Pia ni vizuri kuhakikisha usafi wa kwapa ili kuweza kuhakikisha kuwa,singlet yako inakuwa katika hali ya usafi muda wote na ili isiwe tabu kwako kuinua mkono kwani wengi wanaficha kwapa zao kutokana na uchafu kitu ambacho si kizuri.
Uvaaji huo unazingatia sana rangi kutokana na matakwa ya mvaaji ila wengi wanapendelea rangi nyeupe.
Nguo yoyote ya rangi nyeupe ni nzuri na inapendeza ikivaliwa kwani rangi nyeupe pia huonyesha kipimo cha usafi wako.
Kwa kina dada wanaopenda kuvaa singlet nao wanatakiwa kuhakikisha kuwa kwapa zao zinakuwa safi ili kuweza kuwa huru zaidi.

Jinsi ya kuchagua gauni bomba la harusi


GAUNI bora la harusi ni ndoto ya kila mwanamke anayetaka kuolewa. Kuwa na nguo ya maana siku ya harusi nikitu kizuri ambacho huongeza furaha na kujiamini.
Lakini kabla ya kufanya shoping kwa ajili ya gauni la harusi ni muhimu ukazingatia umbo la bi harusi,rangi yake na mahali ambapo utapata nguo hiyo.
Uchaguzi mzuri unatakiwa kuengana na gharama ya nguo hiyo ambayo hata bi harurusi akivaa ataonekana wa kisasa, anavutia, anajiamini na aliyependeza hilo litamuongezea utulivu.
Nguo nyingi za harusi zimekuwa na gharama kubwa, nunua nguo kulingana na bajeti yako ili usiweze kuharibu mipango mingine.
Kumekuwa na aina mbalimbali za nguo za harusi kulingana na matakwa ya mvaaji na uwezo aliokuwa nao.
Cha muhimu ni kuzingatia nguo hiyo inakuwa bora zaidi na kumpendezesha mvaaji.

Pendeza kwa kuvaa nguo ndefu



WANAWAKE wamekuwa na uchaguzi wa aina gani ya nguo ambayo inatakiwa kuvaliwa katika mtoko wa usiku.
Kuna wale ambao hupendelea kuvaa nguo za kung'aa na wale ambao hupendelea nguo za kawaida lakini zenye mitindo bora zaidi.
Uchaguzi wa nguo inayotakiwa kuvaliwa unatakiwa kuzingatia mambo mengi ikiwemo kuvaa kulingana na tukio husika, kama ni pati ya kawaida au ni kwa ajili ya sherehe fulani.
Uvaaji wako unatakiwa kuzingatia rangi ya nguo na rangi ya mwili wako.
Kama wewe ni mweusi hutakiwi kuvaa nguo nyeusi kwani haitakupendeza, unashauriwa kuvaa nguo za rangi nyeupe,nyekundu, gold, bluu au njano.
Na kama wewe ni mweupe nguo ya rangi nyeusi au rangi nyingine itakupendeza kulingana na rangi ya ngozi yako.
Nguo ndefu ni nzuri zaidi kama zitavaliwa kwa kiatu kirefu na kubeba mkoba mdogo.
Cha kuzingatia ni kuhakikisha kuwa nguo hiyo haikuletei tabu wakati wa kutembea kwani nguo ikiwa ndefu sana husababisha mvaaji kuishikilia na kuonekana wakati mingine kama kituko.
Vaa nguo kulingana na umbo na hata urefu wako, nguo za wazi na ndefu hupendeza sana kama zitavaliwa na mkufu au ushanga shingoni.
Jambo la muhimu ni kuhakikisha kuwa, unakuwa na nguo maalum ya kutokea na unatunza vizuri nguo zako kwani hilo litakusaidia kuongeza umaridadi wako na kujiamini zaidi.

Saturday, January 15, 2011

Umuhimu wa kuvaa hereni


Hereni ni mapambo yanayovaliwa masikioni.
Kuna aina nyingi za hereni katika tamaduni mbalimbali. Heleni hutengenezwa kwa kutumia madini ya thamani kama dhahabu au diamond.
Pia hutengenezwa kwa kutumia silver na almasi.
Lakini pia kwa kutumia ubao, mfupa au kioo, vifuu vya nazi na Kutokana na tamaduni mbalimbali, hereni zimekuwa zikivaliwa zaidi na wanawake, wanaume au jinsia zote mbili.
Mara nyingi uvaaji wa heleni unatakiwa kuzingatia aina ya nguo uliyovaa, hapo unatakiwa kucheza na rangi.
Mpangilio wako wa nguo na hereni hata na viatu utakufanya uonekane maridadi muda wote.
Wanawake wa kimasai wamekuwa wakijipamba kwa mapambo
ya shanga hali ambayo inawafanya wazidi kudumisha
utamaduni wao.
Pia hereni zilizotengenezwa kwa shanga zimekuwa zikiwavutia watu wengi kuvaa kutokana na nakshi yake

Uvaaji wa bangili na maana zake


BANGILI ni kitu kilichotengenezwa kwa lengo la kuvaliwa mkononi kama saa.
Bangili hutengenezwa kwa kutumia ngozi, kitambaa kigumu, plastiki, chuma, na wakati mwingine huwa na nakshi za aina mbalimbali.
Fasheni za bangili hutegemea na matakwa ya mavaaji kwani kuna wale ambao wanapenda kuvaa bangili zilizotengenezwa kwa vito vya thamani kama dhahabu na almasi na wengine wakipendelea kuvaa bangili zilizotengenezwa kutokana na vitu vya asili.
Bangili licha ya kuwa ni urembo wa mkononi, wakati mwingine hutumika kama alama hasa kwa wagonjwa wanapokuwa hospitalini na hutumika kama alama ya mgonjwa.
Hapa nchini kumekuwa na wasanii wa uchongaji ambao
hutengeneza bangili kwa kutumia magome ya miti na wakati mwingine kwa kutumia vifuu vya nazi.
Inaaminika kuwa bangili ambazo hutokana na vifuu vya nazi zimekuwa zikipendeza kuvaliwa kutokana na muonekano wake kwa ujumla na pia huuzwa kwa gharama nafuu ambapo wengi wanamudu kununua kuliko bangili zilizotengenezwa kwa vito vya thamani.
Uvaaji wa bangili pia unatakiwa kuzingatia rangi ya mvaaji, kama mtu ni mweusi anashauriwa kuvaa bangili zenye mng'ao ili kuweza kuwa na muonekano mzuri.
Ni vizuri kama tutazingatia mpangilio wa rangi katika uvaaji wa bangili na itapendeza kama uvaaji huo utazingatia na rangi ya nguo au viatu.

Tuesday, January 11, 2011

Uondoji wa nywele katika maeneo flani

MWANAMKE na hata mwanaume anatakiwa kuwa msafi na si usafi wa kubahatisha.Sehemu ya nywele za siri zimeelezwa kuwa ni sehemu ambapo ngozi yake ni yenye kuhitaji uangalifu mkubwa wakati wa kuziondoa.
Hizi si nywele za kawaida na haziwezi kuondolewa kiholela.Sehemu zinazokaa nywele hizo ni kwapani na maeneo ya faragha.
Kutokana na unyeti wa ngozi katika maeneo hayo watu wa fasheni wamekuwa wakisisitiza kuwa waangalifu zaidi wakati wa kuyafanyia usafi.
Maeneo haya yanatakiwa yaachwe bila mikwaruzo wakati wa marekebisho ya kiusafi yanapofanyika.
Pamoja na kwamba uondoaji wa nywele hizo hauna shida sana wengi wa watu wanapata shida sana baada ya kuondoa nywele husika.
Hii inatokana ama na vifaa vinavyotumika katika uondoaji au ule ukweli wa kawaida kwamba maeneo hayo yanahitaji kuangaliwa kwa makini.
Wengi wetu hunyoa maeneo hayo kwa kutumia nyembe na hii pia huleta matatizo ya kiufundi katika ngozi husika.
Wengine hufanya kitu kinachoitwa Waxing lakini kina maumivu makubwa kwa kuwa nywele huchomolewa kutoka katika kiini chake.
Hata hivyo ukifanikiwa kuondoa unakaa muda mrefu kabla ya kupata shida nyingine.
Ukifanya mwenyewe kazi hii utachanganyikiwa,manake unaweza kuzua uwasho wa kutia aibu kutokana na ngozi yako kukataa kusalimu amri kwakazi yako mwenyewe. Nywele zinazokua ndani huwa tatizo kubwa, njia hii huleta matatizo makubwa.
Unaweza kutumia utaalamu wa kisasa wa kuondoa moja kwa moja nywele hizo, lakini unahitaji fedha na hii ndio shida yenyewe, si kila mtu ana fedha za kufanya mambo hayo.
Uondoaji huu wa kudumu wa kutumia laser huchukua muda mwingi na ama hakika ni miezi kadhaa na hii hakuna mtu anayeitaka.
Bado wapo baadhi ya wanawake ambao wanafanya juhudi za kunyoa na pia kung'oa nywele hizo katika muda mbalimbali.
Lakini pia ukienda kwa wataalamu wanaweza kukupatia vitu vya kuondoa nywele hizo kwa raha kubwa.
Zipo pia kemikali za kuondoa nywele ambapo huzihitaji shauri ni kwenda kwa saluni -zinazohusika.

Ukitaka kunukia kama Rihanna unaweza


UNATAKA kunukia kama Rihana? Inawezekana hujui ananukiaje lakini siku si nyingi utajua binti huyu anayesumbua kwa namna yake ananukia vipi na wewe kama unataka kunukia kama yeye unaweza.
Binti huyu kutoka visiwa vya Barbados anajiandaa kuingiza sokoni manukato yake katika soko.
Hatua yake hiyo inamfanya na yeye kuingia katika msululu wa watu maarufu waliotengeneza manukato yao wakiwamo Britney Spears, Paris Hilton, na Faith Hill.
Manukato hayo mapya yatajulikana kama Reb’l Fleur yanatoa namna ya taarifa na kujenga thamani ya kauli ya binti huyo kwamba bibi yake alizoea kumuita ua lililoasi yaani rebel flower.
Akielezea manukato yake hayo mapya, RiRi anasema: "Nilitaka… kitu kama hiki kwamba ‘Rihanna alikuwa hapa.’ kitu laini, kitu bomba ambacho kinaacha kumbukumbu ya mvuto wa kimapenzi.
"Lakini si kweli kuwa kila mtu anataka kunukia vyema kiasi cha kufikiri kwamba "Rihanna alikuwa hapa,"alisema.

manukato ni biashara ambayo watu maarufu wengi hujiingiza kwani inaonekana hufanya vyema na faida huwa kali.
Watu wengi hununua manukato kwa sababu ya kumpenda mtu anayefanana na manukato hayo hata kama yananukiaje.
Reb'l Fleur itaingia madukani Februari mwaka huu.