Tuesday, August 3, 2010

Are Jelly Shoes Making a Comeback?


The popular 1980s footwear returns with a vengeance
Vile viatu vilivyotamba sana miaka ya 1980,Jelly shoes, vimerejea tena ingawa kwa namna ambayo hata wewe usingelipenda kuvikosa na hakika hata bei yake ni nafuu zaidi.
Jelly shoes are really here again! The 2010 versions are bejeweled, chic and made for adults, with celebs like Anne Hathaway bouncing around in the updated sandals.

Uvaaji wa mikufu na utunzaji wake


NI siku nyingine tena katika urembo na nimeona ni muhimu tukaangalia urembo katika shingo zetu.
Wanawake wengi wenye shingo fupi wana wasiwasi kama kuvaa mikufu kunaweza kufanya waonekane wenye shingo ndefu.
Wabunifu wa mitindo wanasema kuwa, kuvaa mkufu mrefu kunaweza kufanya shingo kuonekana kuwa ndefu.
Wanawake wenye shingo fupi wanashauriwa kuvaa mikufu ambayo inaendana na shingo zao.
Kama unataka muonekano mzuri wa shingo yako unashauriwa kuvaa mikufu ambayo ni inaendana na shingo yako.
Mikufu ya dhahabu imekuwa ikivaliwa sana na kuonekana kuwapendeza wengi Mikufu hii ni ya thamani kubwa ambapo mingine huwa na nakshi za kuvutia.
Lakini si kila mmoja anapenda kuvaa aina hiyo ya mikufu kutokana na kuwa ni ghali sana na wengi wamekuwa hawamudu gharama zake.
Mikufu inayotengenezwa kutokana na silver naye imekuwa ikipendwa na kuvaliwa na watu wengi wa rika zote.
Aina hii ya mikufu imekuwa ikivaliwa zaidi pia na wanaume ambao hupenda kuivaa ikiwa imetengenezwa mithiri ya minyororo midogo.
Uvaaji wa mikufu iunayotengenezwa na dhanga au vitu vya asili kama shamba, vifuu vya nazi na vitu vingine vya asili vimekuwavikivaliwa kwa wingi na wanawake kwa wanaume na kuonekana ni mfano mzuri kwa kutunza utamaduni wa Mtanzania.
Uvaaji wa mikufu hii ya asili huwapendeza zaidi wanawake hasa pale wanapovaa kwa nguo za vitenge huku sehemu kubwa a vazi hili shingoni likiwa wazi.
Mikufu hiyo ina aina ya utunzaji wake ili iweze kudumu zaidi na kuendelea kutunza thamani yake.
Tukianza na utunzaji wa mikufu ya dhahabu, hii inahitaji uangalifu wa hali ya juu ilinapokuja suala la wapi na kwa njia gani mikufu hii inaweza kutunzwa.
Mikufu ya dhahabu inapendeza sana kama ikitunzwa kwenye kasha dogo baada ya kulizungushia kitambaa laini hii husaidia vitu hivyo kutopoteza thamani yake kwa kuhifadhi mng’ao wake.
Hata katika uvaaji wake mikufu hii huitaji kuvaliwa vyema kwa uangalifu mkubwa ili isiweze kushikana na nguo na hatimaye kukatika.
Aina hizo zote za mikufu zinahitaji utunzaji mzuri ili vitu hivyo viendelee kuwa vizuri ikiwemo kuwa na sehemu maalum ya kutunzia mikufu ili kuwa rahisi kwa mvaaji kuitumia mara anapohitaji kuvaa.
Wengi wetu wamekuwa wakitundika mikufu yao ya shanga na plastiki au ile ya asili kwenye stendi maalum iliyotengenezwa kwa ajili hiyo.
Hiyo husaidia sana kwani hata mvaaji hapati shida kujua mkufu wa aina gani unafanana na aina ipi ya nguo pindi anapotaka kuivaa.

Sifa ya mwanamke ni kujipamba


MWANAMKE ni ua. Ni msemo wa muda mrefu ambao tulizaliwa na tukaukuta.
Msemo huu ulikuwa ukimaanisha kuwa, mwanamke atapendeza iwapo atajipamba na kuonekana bomba kila wakati ndiyo maana akafananishwa na maua, hakuna asiyejua thamani ya maua hasa pindi yanapochanua na kuonekana mazuri huku mengine yakitoa harufu nzuri.
Dunia ya leo ni ulimwengu wa wanawake wanaojipamba na kuonekana warembo zaidi.
Wanawake ambao wana uzuri wa asili hasa wale ambao wametunza ngozi zao nyeusi za asili hupendeza sana kama watajipamba kwa vitu vya asili kama kuvaa hereni, mikufu au bangili zilizotengenezwa kwa vitu vya asili kama vifuu vya nazi, magome ya miti au kutengenezwa kwa kutumia shanga.
Wakati huu wanawake wenye uwezo kifedha wamekuwa wakitumia fedha zao kujipamba kwa mapambo ya gharama kubwa kama kuvaa mikufu na saa zenye za dhahabu na hata madini mengine yenye thamani kubwa kama almasi.
Uvaaji wa mikufu, hereni, bangili ni mambo ambayo mwanamke anatakiwa kuyazingatia ili kuweza kuongeza urembo wake.
Wengi wetu tumekuwa tukisahau kutumia vitu hivi katika mavazi yetu.
Vitu hivi vimekuwa vikisaidia sana kuboresha maisha yetu ya urembo kutokana na kuwa unapovaa hereni, mkufu au bangili iliyofanana na nguo uliyovaa hii itasaidia uonekana nadhifu zaidi kuliko unavyofikiri.
Mwanamke ambaye amekuwa akipangilia mavazi yake amekuwa akionekana nadhifu kuliko yule ambaye amekuwa akiweka mwilini kila aina ya rangi na kufanya muonekano wake usiwe mzuri.
Kuna mapoambo mengi siku hizi tena kwa gharama nafuu sana cha kuzingatia ni kucheza na rangi, ukijua namna ya kupangilia rangi za mavazi yako na mapambo yako utakuwa umefanikiwa sana katika kufanikisha muonekano wako uwe mzuri.
Kitu kingine cha kuzingatia ni kuwa, unapoamua kupangilia rangi za mavazi yako hakikisha kuwa mvazi hayo hayawi kwenye rangi za kung’aa sana hasa pindi mavazi hayo ni ya kuvaliwa wakati wa mchana.