Monday, August 31, 2009

NAMNA NZURI YA KUOSHA NYWELE ZAKO



KUNA kitu muhimu kuhusu uoshaji wa nywele, nywele zako ambazo unataka zikae unavyotaka kulingana na kichwa chako ili uwe na uvuto wa haiba yake katika mambo yote yanayokuzunguka.
katika mazingira ya kawaida uoshaji nywele ni kitu cha kawaida na hivyo mara nyingi hatufikirii sana suala la kuosha nywele, si la kawaida tu mwenzangu? Lakini uoshaji nywele wa uhakika wenye makini kwa kutumia shampuu kunaweza kuleta mabadiliko makubwa katika muonekano na umetaji wa nywele zako na hata makuzi yake.
Ndio kusema uoshaji wa kutumia shampuu unaweza kabisa kukupa kile ambacho huwezi kukipata katika hali ya kawaida , muondoko wa ukaaji wa nywele baada ya kuosha.
Lakini kama hutajali tulijadili hili suala la uoshaji nywele ambalo ni la kawaida tu.Naama, la kawaida lakini lenye maana kubwa kwa watu wanaojijali.
Mimi nadhani haitaumkiza kama nikisema kwa ufupi fupi kuhusu hizi shampuu za kuonshea nywele, hizi shampuu ambazo unazipata dukani, kwenye dula la urembo.
Kwanza ni lazima utambue kwamba si kila shampuu inafaa katika kusuklia nyweleza ko (uoshaji) kwani nyingine huleta mushkeri hasa kama unaumwa eczema, hali ya kuchoma choma, uwasho wa nywele, mba au aina ya grisi katika ngozi ya nywele zako wakati wa kuzitengeneza.
Nataka kukuambia kwamba bidhaa zinazotokana na uasili husaidia sana kutengeneza utamu wa nywele kama kweli unaujua na mara zote hufanyakazi bora kwa aina zote za vichwa hata kama zina matatizo niliyotaja hapo juu.
Na pia huleta aina ya burudiko.
Mara zote tunapoosha nywele zetu huwa tunaharibu lakini kama utakuwa mwangalifu kwa kutumia shampuu zenye viambata vya asili (organiki-natural botanical)utakuwa na nafasi kubwa ya kuwa na nywele tamu na wewe kuondokana na adha za uchafu wa nywele unaotia 'wazimu'.
Kama utakuwa huna shampuu ile ya dukani ambayo ina aviambata vya asili nashauri utumie yai. yai ni kifaa kizuri kabisa cha kusafishia.tenganisha kiini cha yai kutoka katika uite mweupe. konga tofauti kisha changanya na taratibu zitumie kuzichanganya katika nywele ne kusukasuka. Acha kwa dakika tatu na kisha safisha kwa maji ya uvuguvugu si ya moto kwani ukitia maji ya moto yao litajikusanya maeneo fulani fulani kichwani halafu itakuwa shida.
Njia tano za kuosha nywele zako:
1.Inama katika beseni. Hii inasaidia kutoa nafasi ya ukaaji mzuri wa kuanza kusafisha nywele bila kuumiza shingo yako na pia kusaidia kuweka damu katika mzunguko unaotakiwa.
2.Tumia kikombe kimoja cha shampuu. Ikiwa nyingi italeta matatizo kidogo na kidogo pia haitatoa kitu kinachostahili. pakaza kwa kusukasuka kila mahali kichwani mwako kwa kuanzia mbele kwenda nyuma na kisha pembeni. Kwa nywele za grisi(mafuta) changanya shampuu na maji kidogo.
3. Tumia ncha ya vidole vyako kufika mwisho wa nywele na kuzimasaji vyema kuhakikisha kwamba shampuu inaingia katika ngozi ya kichwa. Safisha kwa raha kwani inatakiwa ujisikie raha kubwa wakati wa shughuli hii ya kusafisha nywele.
4.Hakikisha kwamba umesafisha sawasawa kichwa chako kisha unaondoa shampuu kwa maji..Kitu cha maana ni kuwa usafishaji lazima ufanyike kwa uangalifu mkubwa kwani baada ya kutia shampuu na kuipeleka kila mahali kuiondoa baada ya hapo ni kitu muhimu.Iondoe kwa maji na kisha kujihakikisha kwamba imeondoka, unastahili kukitia kichwa chako maji ya baridi kwa ajili ya kutoa busti zaidi.
5.Kausha nywele zako kwa taulo safi (kwepa kusugua nywele hizo kwa taulo).Kifunike kichwa na taulo hilo ili linyonye maji taratibu na baada ya hapo unaweza kutia kitu kinachotakiwa ili kuweka nywele za safi.

Miti shamba inayofanya matiti kuwa makubwa na yaliyosimama



MATITI ya mwanamke kuwa katika shepu bomba ni shauri la wanawake wengi na si shauri la mtu mmoja tu. Aidha ni sehemu ya mwili wa mwanamke inayotoa msisimko mkubwa.
Wapo wanawake ambao wana musuli nyingi za matiti na hivyo wanakuwa na matiti makubwa na wengine wana kiasi kidogo na hivyo kuwa na matiti madogo.
Hali hiyo ina sababu zake ingawa wataalamu wanasema kwamba ukubwa wa maziwa huambatana na historia ya familia, umri,kupungua kwa uzito, ujauzito unene na kunyumbuka kwa ngozi ya kwenye matiti, kiwango cha homoni hasa estrogen na progesterone.
kwa kuwa matiti ya mwanamke ni sehemu ya utambuzi wake wa ukike na mwenyewe alivyo na pia ni alama ya uzazi na salama kwa mtoto wake.
Uzuri wa matiti ni kuwa mazima na kama kukitokea kasoro kidogo tu huwa ni kasheshe kubwa kwa upande wa mwanamke. Kutokana na hili nashauri wanawake kuwa na tabia ya kutunza matiti yao ikiwa ni pamoja na kuyakagua na kama kuna kasoro kuyafikisha kwa wahusika kuangalia tatizo.
Usafi wa mwili huambatana na kuyatunza vyema matiti yako.
Lakini wengi wanaotaka matiti makubwa ndio ho wanaopata adhabu ya kusaka matiti hayo kwa udi na uvumba.
Uzuri wa matiti
zipo njia nyingi za kuwa na matiti bomba na kwa sasa duniani matiti bomba ni yale makubwa( nadhani hii ni fasheni).Unaweza kupata matiti hayo kwa upasuaji au na kwa kupachika kitu ndani hasa silikoni na nyingine ni kutumia dawa ambapo misuli hujazia na kuyafanya matiti kuwa makubwa.
Njia ya kukuza matiti kwa salama ni kutumia dawa ambazo zimetolewa katika miti shamba, mitishamba ambayo ikichanganywa pamoja inafanyakazi mbalimbali ya kuboresha ukubwa na uimara wa matiti.
Mitishamba hii inatoka sehemu mbalimbali na Afrika Kusini wamefanikiwa kutengeneza dawa kutokana na miti hii na wanaotaka urembo wa matiti makubwa na yenye kuonekana wanapata nafasi kubwa ya kununua dawa hiyo.
Aidha baada ya kujazia matiti yako na kuwa makubwa kitu kinachofuata ni kuhakikisha kwamba matiti yako hayalegei na kuwa katika ukubwa wake bado yanasimama katika saa inayotakiwa na yenye raha yake si kutazama bali pia kuyatomasa.
Matiti hupendeza zaidi baada ya kuonekana yakiwa yametulia na yanayokubali brasia zenye maana duniani.
Aidha uzuri mwingine utatokana na kuwezesha matiti yako imara kwa kufanyia hali ya kuwezesha musuli za maziwa kufanyakazi yake.
Pamoja na kuongeza ukubwa wa matiti ni vyema kama ngozi yako inakuwa na rangi ile inayofaa huku ukihakikisha kwamba chini ya maziwa jacho halikai na wala brasia haisababishi wewe kuwa na kazi ya ziada katika usafi wa eneo hilo.
Ipo haja ya kutumia mafuta yanayostahili kukata mnururisho mkali wa mwanga unaoweza kusababisha kansa ya ngozi.
Kliniki moja ya Afrika Kusini St Herb Beauty Breast Care imetengeneza aina fulani ya mitishamba yenye mchanganyiko maridhawa kwa ajili ya matumizi ya wanawake wanaotaka urembo wa matiti makubwa na yaliyosimama bila upasuaji wala kutumbukiza kitu katika matiti hayo.
Ni lazima kuwe na mizania ya mitishamba kupata kile kitu unachotaka. Kliniki hiyo imekuja na fomula yake inayoitwa Beauty Bust Herbal Breast Enlargement Formula ambayo hushawishi kukua kwa misuli za matiti bila kushawishi uzalishaji wa maziwa na kuyaongezea uzuri matiti yako.
Pamoja na matiti hayo kuwa bora kwa matumizi hayo, matiti makubwa hulainika sana unapokuwa mzee na hili ndilo hasa nililotaka kusema, mazoezi ya mwili husaidia sana bado kuweka matiti katika shepu yake.
Kama u kijana na matiti yako yanakuwa malapa basi huenda tatizo si tu musuli zimelegea bali pia huvai brasia kukusaidia. maziwa yanaweza kuwa malapa kwa kutokuwa na kitu cha kusaidia kusimama.Hili ni wazi zaidi kwa wanawake wenye matiti makubwa au watu ambao wanafanya mazoezi bila kuwa na sapoti ya brasia.Pia matiti yanaweza kuwa malapa kutokana na kujifungua
Lakini ukitaka uhakika wa uzuri wako kwa namna ya kuwa na matiti makubwa na yalioyosimama vyema ni lazima utumie dawa hizi za matishamba ambapo mchanganyiko wake ndio umetoa fomula ya St Herb :
Fenugreek :
Kwa kawaida matunda ya mmea huu yalikuwa yanatumika na wanawake wa Kigiriki kuongeza ukubwa wa matiti yao na imehakikishwa kisayansi kuwa mtishamba huu huongeza athira ya mastogenic kwa misuli inayotengeneza maziwa.
matunda( mbegu ) ya mtuii huo yalikuwa yanatengeneza aina ya dawa ijulikanayo kama phytochemical diosgenin na estrogenic isoflavones zinazooongeza utengenezaji wa dawa ya estrogen katika mwili, dawa ambayo ni ufunguo kwa matiti yenye shepu ya mchonoko na yaliyojaa.
Mmea wa Saw Palmetto:Huu ni mmea wa kaskazini mwa Marekani na kwamba unafanana na mtende ni moja ya mmea wenye kemikali chache unaotengeneza musuli na husawazisha matatizo ya mkaziwa yenyewe.
Fennel Seed:Husaidia kuzalisha musuli nyingine mpya
L-Tyrosine:Hii ni amino acid, Tyrosine ambayo hudhibiti uzalishaji wa homoni na hivyo kupunguza unene na.
Mexican Wild Yam:Matumizi ya kila siku yanapunguza michirizi isiyotakiwa katika matiti.
Kelp:Ni zao la baharini. Ni chanzo bora cha madini ya iodine chakula chenye hiki huleta homoni zilizojipanga vyema.
Damiana:Kikawaida hutumika kwa ajili ya kuleta mizania ya homoni.Kuleta ukuzi mwema wa matiti, kupunguza dalili za matatizo yanayoambatana na siku za hedhi na kuchanganya ashiki;husaidia kupunguza uzito kuleta nguvu na kuondoa uchovu.
Dong Quai:kikawaida mmea huu wa Asia hutumika kuripea seli ikiwemo ya mammorianna, (tezi za matiti).
Mother's Wort:Mmea uliopo sehemu nyingi za Ulaya na kandoni mwa mito ambazo hutoa msukumo fulani katika kano la uzazi.
Black Cohosh :Mmea unaopatikana kaskazini mwa Marekani hutumika kama dawa ya kubadilisha homoni.
Avena Sativa:Ni kama shayiri na ina kiasi kikubwa cha saponins, flavonoids, minerals, na alkaloids kwa ajili ya mfumo wa homoni.
Humulus Lupulus:Husaidia kuimarisha matiti.
kisasili cha matiti
1. Kujiamini kwa mwanamke kumejikita zaidi katika ukubwa wa matiti yake
2. Wanawake hawana muwashawasha sana na ukubwa wamatiti yao
3. Brazia za kimichezo si za lazima.
4. matiti makubwa yanauhusiano na mambo ya ngono
5. Wanawake na matiti madogo hushindwa kunyonyesha kwa ufanisi
6. Wanawake wote hufurahia kutomaswatomaswa kwa matiti yao
7. Wanawake kwa kawaida huwa na matiti mawili yenye ukubwa unaofanana
8. Nywele kuzunguka chuchu huonyesha kwamba mwanamke huyu si wa kawaida
9. Wanawake na matiti makubwa ni wazazi sana
10.Unyonyeshaji husababisha matiti kuwa malapa

Wednesday, August 26, 2009

umuhimu wa afya ya nywele



Kuna mambo mengi ya kufanya katika kuhakikisha kuwa nywele zako zinakuwa zenye afya.
Mtaalam kutoka Chicago healers Comina DK Melody Hart anasema kuwa, afya ya nywele inategemea sana mzunguko wa damu na lishe.
Pia inaweza kutokana na homoni na tezi, ni vyema kuangalia kwa mtindo fulani wa maisha yanavyokwenda wakati unaona hakuna kasoro katika nywele zako.
Shauri kubwa ni lishe. Ni vyema kuangalia chakula tunachokula kama tunahitaji afya ya nywele zetu.
Sehemu kubwa ya vyakula tunavyokula havina vitamini, madini, wala antioxidants kwa mfano kula vyakula organic husaidia sana afya ya nywele, anasema Dk. Julia Tatum Hunter.
Dk.Hart anashawishi kula vyakula vyenye silica na sulphur kama vitunguu, vitunguu swaumu, mboga za kijani na mayai.
Sulphur inajulikana kwa msaada wake kwa nywele, ngozi na kucha.
Watu wenye upungufu wa sulphur vyakula vyenye lodin na potassium kama mwani husaidia kukua kwa nywele na unene wake.
Unatakuwa kupunguza ulaji wa vitu vitamu kama pipi, soda, sukari, chumvi na kahawa katika mwili kama mtu anataka kustawisha nywele.
Badala ya kunywa soda na kahawa mtu anastahili kunywa maji kwa wingi. Mwili unatengenezwa na asilimia 60 mpaka 80 na maji.
Kama utanyimwa maji afya ya chembe hai zitakuwa katika mgogoro mkubwa.Ukosefu wa maji hukosesha ukuaji wenye afya wa mwili . Kimsingi unashauriwa kutumia glasi sita za maji kwa siku.

Tuanzie busati letu na urembo wa asili
















Hizi ni picha za mapambo mbalimbali yanayoamgusa mwanamke. Unaweza ukaona mwenyewe yanavyochukua nafasi mbalimbali katika maungo yako kutoka kichwani hadi mguuni na pasi shaka katika sebule. Kila mara tutafanya kitu fulani kukumbushana.

Karibuni katika busati la utanashati na urembo

Nimeamua kuanzisha gazeti tando hili kuchangia kwenye ulimwengu wa elimu kuhusu miili yetu utanashati na urembo mchango tunaukaribisha