Tuesday, January 11, 2011

Uondoji wa nywele katika maeneo flani

MWANAMKE na hata mwanaume anatakiwa kuwa msafi na si usafi wa kubahatisha.Sehemu ya nywele za siri zimeelezwa kuwa ni sehemu ambapo ngozi yake ni yenye kuhitaji uangalifu mkubwa wakati wa kuziondoa.
Hizi si nywele za kawaida na haziwezi kuondolewa kiholela.Sehemu zinazokaa nywele hizo ni kwapani na maeneo ya faragha.
Kutokana na unyeti wa ngozi katika maeneo hayo watu wa fasheni wamekuwa wakisisitiza kuwa waangalifu zaidi wakati wa kuyafanyia usafi.
Maeneo haya yanatakiwa yaachwe bila mikwaruzo wakati wa marekebisho ya kiusafi yanapofanyika.
Pamoja na kwamba uondoaji wa nywele hizo hauna shida sana wengi wa watu wanapata shida sana baada ya kuondoa nywele husika.
Hii inatokana ama na vifaa vinavyotumika katika uondoaji au ule ukweli wa kawaida kwamba maeneo hayo yanahitaji kuangaliwa kwa makini.
Wengi wetu hunyoa maeneo hayo kwa kutumia nyembe na hii pia huleta matatizo ya kiufundi katika ngozi husika.
Wengine hufanya kitu kinachoitwa Waxing lakini kina maumivu makubwa kwa kuwa nywele huchomolewa kutoka katika kiini chake.
Hata hivyo ukifanikiwa kuondoa unakaa muda mrefu kabla ya kupata shida nyingine.
Ukifanya mwenyewe kazi hii utachanganyikiwa,manake unaweza kuzua uwasho wa kutia aibu kutokana na ngozi yako kukataa kusalimu amri kwakazi yako mwenyewe. Nywele zinazokua ndani huwa tatizo kubwa, njia hii huleta matatizo makubwa.
Unaweza kutumia utaalamu wa kisasa wa kuondoa moja kwa moja nywele hizo, lakini unahitaji fedha na hii ndio shida yenyewe, si kila mtu ana fedha za kufanya mambo hayo.
Uondoaji huu wa kudumu wa kutumia laser huchukua muda mwingi na ama hakika ni miezi kadhaa na hii hakuna mtu anayeitaka.
Bado wapo baadhi ya wanawake ambao wanafanya juhudi za kunyoa na pia kung'oa nywele hizo katika muda mbalimbali.
Lakini pia ukienda kwa wataalamu wanaweza kukupatia vitu vya kuondoa nywele hizo kwa raha kubwa.
Zipo pia kemikali za kuondoa nywele ambapo huzihitaji shauri ni kwenda kwa saluni -zinazohusika.

2 comments:

  1. Asante kwa mada nzuri, hizo dawa zngne za ktuoa nywele pamoja na laser hua znapatikana kwa bei gan na majina yale plz?? Hazina madhara?

    ReplyDelete