Thursday, August 27, 2015

Uvaaji sketi fupi uzingatie utamaduni wetu


UVAAJI wa sketi fupi mara nyingi hutegemea na matakwa ya mavaaji,


 kwani mara ntingi sketi fupi huishia juu ya magoti na huwa na urefu usiozidi sentimita 10.
Vazi hili mara nyingi huvaliwa na wanawake wa nchi za magharibi pia utamaduni huu umeenea sana hapa nchini ambapo wanawake na wasichana wengi wamekuwa wakivaa aina hizi za nguo na kuonekana kuwa wanakiuka maadili ya Kitanzania.
Wataalam wa mavazi wanasema, chimbuko la sketi fupi ni huko London Uingereza katika miaka ya 1960 ambapo wanawake walikuwa wakivaa nguo hizo katika michezo mbalimbali na wakati huo nguo fupi zilikuwa zikijulikana kama nguo za michezo kwani zilikuwa zikivaliwa sana na wacheza tenisi.
 Wengi wanaovaa aina hiyo ya nguo wamekuwa na sababu tofauti huku wengine wakidai kuwa vazi hili hufanya wajiamini zaidi huku wengine wakidai kuwa sketi fupi hufanya wajione bomba zaidi na kuonekana wanakwenda na wakati.
Sketi fupi zipo kwenye fasheni miaka nenda rudi japo watu wengine wamekuwa wakivaa nguo hizo zikiwa fupi sana na kuleta mtafaruku hata pale wanapokuwa wanapita barabarani.
Muhimu kuhakikisha kuwa unapochagua nguo ya kuvaa angalia kama inaendana na mazingira na utamaduni wa Mtanzania na je nguo yake umevaa mahali gani na kama unaona ni kero unapofanya hivyo basi unashauriwa kuacha kufanya hivyo.
Wengi wanavaa sketi fupi na viatu virefu huku wakitembea umbali mrefu hali inayosababisha kupoteza maana na heshima pia.
Vaa nguo kulingana na mazingira, kama una gari ni sawa lakini kama unajua unakwenda kutumia usafiri wa daladala huku ukiwa umevaa sketi fupi itakayokufanya ushindwe kukaa vizuri na hata kuinama hiyo si sawa sawa.


No comments:

Post a Comment