Thursday, August 27, 2015

Unene husababisha muda mfupi wa kuishi



Uzito ni sawa na uvutaji wa sigara ambao huleta matatizo makubwa kwa watu ambao wamo katika kilinge hicho.

Wataalam wa afya na urembo wanasema wazi kuwa mnene kunapunguza sit u namna ya kujiweka sawa katika masuala mbalimbali ya kijamii lakini pia unakuwa na muda mfupi sana wa kuishi duniani.
Wataalam wanasema kwamba kuwa mzito kunapunguza maisha yakokwa miaka mitatu anasema mtafiti Gary Whitlock kutoka Clinical Trial Service Unit ya Chuo Kikuu cha Oxford  kilichopo
Uzito huo ni ule unaokuwa mara tatu ya uzito ambao mtu anatakiwa awe nao kutokana na urefu wake, umri na afya yake.
Ndio kusema kama mtu anakuwa na uzito mathalani paundi 150 mtu huyo anapunguza umri wake wa kuishi duniani kwa miaka 10.
Pia uzito wa kuchusha umekuwa ukileta tatizo la figo, ini na aina kadhaa za kansa na pia huleta matatizo ya magonjwa ya moyo na kiharusi.
Unene huleta mchosho mkubwa kwa moyo na huleta mizania dhaifu ya rehemu na kusababisha shida katika mwenendo wa damu.
Wakati wanaume wenye kiuno kikubwa huongeza hatihati ya kifo wakati wanawake wenye mzunguko mkubwa huongeza hatihati ya kifo kwa asilimia 78

1 comment: