Thursday, December 26, 2013

'Urembo si sura nzuri tu ni pamoja na kujituma'


MSHINDI wa Pili wa taji la Miss Utalii Mkoa wa Dodoma mwaka 2011, Jackline Leshange amesema urembo  ni pamoja na kujituma.
“Urembo bado naupenda na sitaacha urembo, napenda hata mavazi ninayovaa yanitambulishe kuwa ni mrembo. Urembo si sura nzuri tu lazima ujue kujituma na kujiweka nadhifu”
Jackline amesema aliingia kwenye urembo mwaka 2010 kutokana na kupenda fani hiyo na alikuwa akifuatilia warembo mbalimbali kwenye Televisheni na hata kwenye majarida mbalimbali.
Mara ya kwanza kushiriki masuala a urembo ilikuwa ni Juni 2011, alipojitosa kwenye mashindano ya Miss Dodoma ambapo hakufanikiwa kuingia kumi bora.
“Sikukataa tamaa  Oktoba mwaka 2011 nilishiriki mashindano ya Miss Utalii Dodoma ambapo niliibuka mshindi wa pili”

Anasema  kwa sasa licha ya kujishughulisha na kazi ndogondogo za kujiingizia kipato pia jioni anakwenda darasani ili kujiendeleza zaidi kielimu.


Jackline akiwa katika pozi

Jackline Leshange

Jackline Leshange akiwa amepozi


No comments:

Post a Comment