Saturday, January 15, 2011

Umuhimu wa kuvaa hereni


Hereni ni mapambo yanayovaliwa masikioni.
Kuna aina nyingi za hereni katika tamaduni mbalimbali. Heleni hutengenezwa kwa kutumia madini ya thamani kama dhahabu au diamond.
Pia hutengenezwa kwa kutumia silver na almasi.
Lakini pia kwa kutumia ubao, mfupa au kioo, vifuu vya nazi na Kutokana na tamaduni mbalimbali, hereni zimekuwa zikivaliwa zaidi na wanawake, wanaume au jinsia zote mbili.
Mara nyingi uvaaji wa heleni unatakiwa kuzingatia aina ya nguo uliyovaa, hapo unatakiwa kucheza na rangi.
Mpangilio wako wa nguo na hereni hata na viatu utakufanya uonekane maridadi muda wote.
Wanawake wa kimasai wamekuwa wakijipamba kwa mapambo
ya shanga hali ambayo inawafanya wazidi kudumisha
utamaduni wao.
Pia hereni zilizotengenezwa kwa shanga zimekuwa zikiwavutia watu wengi kuvaa kutokana na nakshi yake

No comments:

Post a Comment