Thursday, October 22, 2009

Uzito mkubwa si sahihi kwa afya na urembo wako


TUMEKUWA kila siku tukizungumzia masuala ya kuweka ngozi safi na sura bomba lakini mara zote huwa tunasahau kuzungumzia uzito ambao ama hakika ni kitu kibaya kuliko kitu chochote kile.
Uzito ni sawa na uvuitaji wa sigara ambao huleta matatizo makubwa kwa watu ambao wamo katika kilinge hicho.
wataalamu wa afya na urembo wanasema wazi kuwa kuwa mnene kunapunguza sibtu namna ya kujiweka sawa katika masuala mbalimba;li ya kijamii lakini pia unakuwa na muda mfupi sana wa kuishi duniani.
Wataalamu wanasema kwamba kuwa mzito kunapiunguza maisha yako kwa miaka mitatu anasema mtafiti Gary Whitlock kutoka Clinical Trial Service Unit ya chuo kikuu cha Oxford kilichopo nchini Uingereza.
Uzito huu ni ule unaokuwa mara tatu ya uzito ambao unhatakiwa mtu awe nao kutokana na urefu wake,umri na pia afya yake.
Ndio kusema kama mtu anakuwa na uzito mathalani paundi 150, mtu huyu anapunguza umir wake w akuishi hapa duniani kwa miaka 10.
Sasa kama unapunguza umri huo watu wako wanakupenda wtafanaya nini.
Kwa maelezo mengine ni kuwa uzito wa aina hii ni sawa na uviutaji wa sigareti ambapo pamkoja na kuchakaza ngozi pia hupunguza maisha ya mtu kwa miaka kumi.
Ndio kusema katika urembo pamoja na kupiga vita sigareti uzito wa kuchusha nao lazima upigwe vita.
Kwa wanawake wengi wa kiafrika wanadhani kuwa mnene ni kuonekana bomba, pamoja na kuwa mnene ni kutamu kwani unakuwa na nyama za kushikwa lakini ni vyema watu wakatambua kwamba uzito wa kuchusha yaani mara tatu ya ulke unaostahili kuwa nao ni hatari kubwa kwa maisha yako.
Onyo hili la wataalamu limefanywa baada ya uchunguzi kwa watu 894,576 waumde kwa wake katika tafiti 57 zilizofanywa.
ingawa tafiti hizi zilifanywa kwa watu wa Kaskazini mwa Marekani na Ulaya kwa watu wenye ujazo wa 25 (BMI) hata hapa nchini watu wanastahili kuangalia juzito wao.
Kwa taarifa yako uziuto wa kuchusha hule ta tatizo la figo, ini na aina kadha za kansa na pia hyuleta matatizo ya magonjwa ya moyo na kiharusi. Unene huleta mchosho mkubwa kwa moyo na pia kuleta mizania dhaifu ya rehemu na kusababisha shida katika mwenendo wa damu.
Wanaume wenye kiuno kikubwa huongeza hatihati ya kifo wakatiw nawake wenye mzunguko mkubwa huongeza hati hati ya kifo kwa asiulimia 78.

No comments:

Post a Comment