Wednesday, October 21, 2009

mambo yanayofaa kwa miguu minene


Ni kasheshe kubwa kuirembesha miguu mikubwa, lakini ni kweli kuwa unahitaji miguu yako hiyo kuwa na nafasi kubwa ya kuonyesha uzurui ulionao.Kipendezacho ni chako.Miguu mikubwa si mwisho wa fasheni unachotakiwa kujua ama hakika ni namna ya kuiweka vyema miguu yako na uonekane bomba.
Wapo watu ambao wamekuwa na miguu mikubw akutokana na sababu mbalimbali na pamoja na kuwa na miguu hiyo wka sababu ama z alishe au kutofanya mazoezi wewe kama binti au mke unataka nguo zako zisiwe na ubazazi na badala yake zionyeshe raslimali ulizonazo yaani uzuri wako.
Kama unataka kuweka miguu yako mikubwa katika hali bora ni lazima uanze kula lishe njema na pia kufanya mazoezi.
Kitu kingine kizuri kwa wewe mwenye miguu mikubwa au tuseme minene ni kuhakikisha kqamba unavaa nguo zinazofiti lakini nguo zinazobana sana si nzuri hata kidogo na zilizopana kabisa nazo mbaya kwani itaonekana mkiguu yako ni mikubwa sana kuliko unavyofikiri.
Wakati unavaa suruali mathalani, vaa ile ambayo ni pana ambayo haipigii tambo miguu yako.
na kama ni viatu lazima uwe unavijulia kwelikweli hata siku moja usivae buti na sketi ambayo inaonyesha miguu yao waziwazi.
nataka kusema hivi kuwa na miguu minene au tuseme mikubwa si tatizo, tatizo ni wewe namna unavyofanya mambo na namna unavyojiweka katika maizngira ya kupendeza na nguo zako za kupendeza ambazo hazibani wala hazipwai.
Na pia unaweza kwa namna nzuri kabisa kuachana na sketi na pensi nyanya ambazo zinakata laini ya miguu yako kama enka nakadhalika.
tengeneza staili ambayo utaonekana wa kawaida na u mrembo katika hilo.

No comments:

Post a Comment