Sunday, September 6, 2009

Chumvi,sukari nyingi huzeesha ngozi


Shosti niwaambieni kuwa matumizi makubwa ya chumvi au sukari ni hatari na sumu kubwa katika ngozi zetu kwani husababisha ngozi kuwa na makunyanzi kabla ya umri.

Kawaida makunyanzi hutokea unapokaribia kuimaliza miaka ya 40.Watu ambao ngozi zao zimeathiriwa na matumizi makubwa ya sukari na chumvi wanashauriwa kupunguza matumizi yavitu hivyo kwa kula mboga za majani na matunda kwa wingi ili kuweza kuondoa sumu ambayo imejengekamwilini na pia kunywa maji mengi.

Wanasayansi wanasema kuwa, watu wanaotaka kutunza ngozi zao kutotumia sukari kwa wingi kwani sukari huchangia kuzeesha ngozi. Sukari nyingi hufanya misuli ya protini katika ngozi kujikusanya pamoja na kusababisha kutoweka kwa mnyunyuriko unaotakiwa.

Ili ngozi iwe laini ni yema ukanywa maji mengi, maji husaidia kulainisha miili yetu kwani mwili unapokuwa hauna maji ya kutosha unakuwa mkavu na ngozi haipendezi hata kama unatumia vipodozi vya aina mbalimbali na vya gharama. Ni bora kuulisha na kuunywesha mwili wako ili ngozi ijitengeneze yenyewe.

No comments:

Post a Comment