Wednesday, August 26, 2009

umuhimu wa afya ya nywele



Kuna mambo mengi ya kufanya katika kuhakikisha kuwa nywele zako zinakuwa zenye afya.
Mtaalam kutoka Chicago healers Comina DK Melody Hart anasema kuwa, afya ya nywele inategemea sana mzunguko wa damu na lishe.
Pia inaweza kutokana na homoni na tezi, ni vyema kuangalia kwa mtindo fulani wa maisha yanavyokwenda wakati unaona hakuna kasoro katika nywele zako.
Shauri kubwa ni lishe. Ni vyema kuangalia chakula tunachokula kama tunahitaji afya ya nywele zetu.
Sehemu kubwa ya vyakula tunavyokula havina vitamini, madini, wala antioxidants kwa mfano kula vyakula organic husaidia sana afya ya nywele, anasema Dk. Julia Tatum Hunter.
Dk.Hart anashawishi kula vyakula vyenye silica na sulphur kama vitunguu, vitunguu swaumu, mboga za kijani na mayai.
Sulphur inajulikana kwa msaada wake kwa nywele, ngozi na kucha.
Watu wenye upungufu wa sulphur vyakula vyenye lodin na potassium kama mwani husaidia kukua kwa nywele na unene wake.
Unatakuwa kupunguza ulaji wa vitu vitamu kama pipi, soda, sukari, chumvi na kahawa katika mwili kama mtu anataka kustawisha nywele.
Badala ya kunywa soda na kahawa mtu anastahili kunywa maji kwa wingi. Mwili unatengenezwa na asilimia 60 mpaka 80 na maji.
Kama utanyimwa maji afya ya chembe hai zitakuwa katika mgogoro mkubwa.Ukosefu wa maji hukosesha ukuaji wenye afya wa mwili . Kimsingi unashauriwa kutumia glasi sita za maji kwa siku.

No comments:

Post a Comment