Wednesday, January 20, 2010

Vivazi vyenye mvuto


KUNA mavazi ya aina nyingi ambapo yakivaliwa humfanya mtu apendeze au achukize Uvaaji wa nguo unatakiwa kuzingatia umri na rangi ya mwili na pia mazingira ya nguo inapovaliwa.
Sio kila nguo ni ya kuvaliwa mchana na si kila nguo ni ya kutoka nayo barabarani aina nyingine ya nguo haistahili kuvaliwa barabarani.
Mathalani wewe ni mfanyakazi unajua unatakiwa uvaeje, kujiweka mrembo na mtanashati ni muhimu pia .
Uvaaji wa nguo zilizopangiliwa rangi zinazoenda sambamba na mkoba na viatu, utengenezaji mzuri wa nywele ni muhimu.
Kuvaa nguo zenye machanganyiko wa rangi mara nyingi huonekana kuwa na muonekano mbaya hata kama nguo hizo ni za gharama kubwa. endelea kupangilia rangi y nguo iende sambamba na kiatu na mkoba.
Vaa kulingana na mahali na wakati. Kuna nguo za kazini na za kutokea. Unaponunua na kuvaa nguo ya kitoto wakati wewe ni mzee unakuwa na maana gani?
Unaweza kuwa na miaka 50 na usafiri bomba je upo tayari kuvaa kimini kikali? Sina hakika lakini ni vazi hilo ni shauri lako na huenda ukawa ni samaki katika nchi kavu kwa kuangalia tamaduni zetu.
Kizazi cha sasa kinarekebisha sana masuala ya mavazi ndio maana nataka kusema kwamba shauri la staili si lile la una miaka 50 unataka kushindana na binti yako mwenye miaka 20.
Kwa umri wako wa miaka 50 unaweza kutafuta mavazi yenye mvuto kulingana na umri wako na ukatoka bomba vile vile.
Mavazi ni muhimu yakazingatia umri

No comments:

Post a Comment