Wednesday, July 30, 2014

Tengeneza mwili wako kwa kunywa maji ya Aloe Vera

Kwa ukweli kuna mshindani mpya wa maji yanayorekebisha mwili wako na kuonekana mrembo zaidi. Watu wa urembo ambao walikazania unywaji wa maji ya dafu sasa wana kitu kipya mtaani, kinywaji cha aloe vera.

Aloe vera wataalamu wanasema kwamba ikinyweka katika maji inasaidia sana kuyeyusha chakula, kuondoa sumu zilizomo mwilini na kuondoa kiungulia lakini kubwa zaidi linabortesha muonekano wako.

Wataalamu wanasema pamoja na kuleta lishe katika mwili kuondoa tatizo la maji kwa ajili ya mwili na ngozi pia ina homoni mbili za Auxin na Gibberellins ambazo huleta kinga dhidi ya viungulia na pia kuleta uponyaji.

Kauliu hiyo imetolewa na mwasisi wa Sublime Beauty, Kathy Heshelow, Gibberellins zinaaminika kuchochea ukuaji wa seli mpya kwa kuimarisha fibroblasts amnbazo hutengeneza collagen.

Maji haya husafisha tishu za ngozi ambazo huathirika sana na sukari na pombe.

Mwili unapokuwa msafi na ngozi nayo inakuwa safi na  maji haya yanasaidia sana kuufanya mwili kuwa bora.

Maji ya aloe vera yanapatikana katika maduka makubwa lakini waweza tengeneza kwa namna hii:
chukua aunzi moja ya juisi changanya na aunzi nane za maji kila siku.

Saturday, July 19, 2014

Tumia asali kufanikisha urembo wako

Nauza asali mbichi ambayo haijachanganywa na chochote ni nzuri kwa ngozi na afya yako. Bei ni Sh. 10,000 kwa kilo moja na Sh. 5,000 kwa nusu kilo.
Mawasiliano 0719818644/0762650760










Mtaalam mmoja wa ngozi mwenye makazi yake mjini New York City ambaye pia ni daktari, Amy Wechsler anasema hali ya kunyunyurika iliyonayo asali na inayonasa inafanya kuwa kinga imara katika kidonda ambacho kinahitaji kisiingiliwe n vimelea na kutoa mazingira ya kuponya, hivyo asali ni bomba kwa tiba.

 Pamoja na tiba asali ni moisturize babu kubwa kwa ajili ya sura na mwili pia.
Asali ni dawa ya asili ambayo ina uwezo wa kukusanya maji  kutoka ndani ya misuli hadi katika sehemu za juu a ngozi na hivyo kusaidia kuondoa mikunjo.

Mimi nakushauri jaribu moisturizing ya asali ambayo itaondoa ukavu wa ngozi yako na hata kuwasha na kutatarika.

Changanya vijiko vya mezani viwili vya asali na vijiko viwili vya mezani vya maziwa.
Kisha pasha moto mchanganyiko huo, kisha paka mchanganyiko huo katika uso wako na kupumzika kwa dakika kama kumi hivi.
Kisha jioshe kwa maji ya vuguvugu.Kama unataka kitu kama kosmetiki agiza lotion ya asali ili kuweka sawa ngozi yako.
Hakikisha unanunua lotion ambayo imetengenezwa kwa asali isiyochujwa.
Aina zote za asali zinasaidia kuondoa mikunjo ya uzeeni.