Thursday, October 22, 2009

makosa tunayofanya katika kufanya urembo wetu


KUNA makosa mengi sana yanafanywa na watu katika juhudi za kubaki mrembo au kusaka urembo. makosa haya mara nyingi yanaleta matatizo makubwa hasa katika ngozi , macho au katika kichwa.
mara nyingi shughuli hizi za urembo wanawake hujikuta ama wanapitiliza au wanafanya kinyume na kutaka matokeo ya haraka na matokeo yake ni msheshe.
Mambo yanayoharibu katika urembo ni pamoja na kutokuangalia fiziki yaani kutofanya mazoezi. Hata kama hakuna mtu ambaye atakuona kuacha kufanya mazoezi, kutojali usafi kunatibua muonekano wako na kuondoa kujiamini.
Kitu kingine ambacho watu huwa hawakijali ni kusafisha na kurekebisha meno yao. Unapotabasamu kitu cha kwanza kuonekana kwa watu ni meno yako. basi jaribu kuyajali kidogo. yasafishe na hakikisha yanapendeza.
Kitu kingine ambacho huwa watu hawajali ni kuhakikisha kwamba mikono yao i safi na isiyokuwa na mikwaruzo. Usisahau kuitia mikono yako losheni na kuweka kucha zako safi na zinazopendeza na rekebisha kucha hizo.
Usizivuruge sana kope zako, jaribu kutafuta kitu kitakachopendezesha kope zako na kama kuna makosa usizigandamize bali weka kinachotengeneza uonekano safi.
Kuwa mwangalifu na vitu unavyotengeneza au unavyodhani vinafaa kw aurembo wako. vingine vina aleji viogope. na ukipata aleji usikimbilie kujaza kitu kingine bali angalia nini na tafuta suluhu yake kwanza.
La maana ni kuwa ni vyema kujaribu kwanza kitu katika kiganja au mkono mahali padogo kabla ya kuanza kutumia inavyostahili hasa kwa bidhaa unazotengeneza mwenyewe.

Vyakula vya kuleta ashki

Moja ya vitu ambavyo humfanya mtu kuwa na furaha na maisha mazuri ni ubashashi unaombatana na kuondoka kwa mikonjo ya moyo kwa kupata huduma ya ngono.
Nyingi ya dawa zinazoleta hamu ya ngono puia husaidia kurekebisha mfumo wa afya ya mwanamke, ndio maana nimetaka kwa hapa kidogo kuzungumzia vyakula vya kuleta ashki
Watafiti wamesema kwamba kuna aina fulani ya vyakula huleta ashki kubwa kiasi cha kuwafanya watu wawe na hamu ya kufanya ngono.
Vyakula hivyo vimedaiwa kuwa na aina fulani za kemikali ambazo hufumua mifumo ya tamaa na kufanya dai la kufanya ngono kuwa na nguvu zaidi.
Kutumia chakula kitamu kwa upungufu na kupata lishe kamili yenye uhakikakunaweza kukufanya wewe kufurahia ngono na kutamani kama masuala hayo yameanza kukimbia.
Yaani ukipata dozi inayotakiwa ya protein, carbs, na fats ni dhahiri utakuwa na nguvu zaidi kuliko hapo awali.
Lakini kabla sijakuchanganya zaidi natakakusema kwamba kuwa na nguvu ni kitu kingine na kuwa na hamu ya kufanya ngono na kuimudu ni kitu kingine.
Yaani ukiwa na uwezo wa kufanya mapenzi na kuwa na nia ya kufanya mapenzi kunatokana na wakati wmingine na aina ya chakula unachokula.
Wazungu wanasema kwamba vipo vyakula ambavyo kwa mchanganyiko wake vinbatoa kitu kinachoitwa kwa kizungu aphrodisiacs, yaani vitu ambavyo vinapandisha libido na kuachia tamaa kubwa ya ngono.
Vyakula hivi vinapunguza rehemu vinaweka sawa kiwanda cha kufanya mapenzi, vinaleta riha nzuri zaidi na kuweka homoni katika namna ambayo inastahili.
Pamoja na kukuongezea hizo hamu lakini vyakula hivyo pia vinatoa nishati ya kukutosha kufanya mapenzi.
Wapo waswali wanaokula ngisi, wapo wanaokula karanga, wapo wanaokula muhogo mbichi, wapo waanaolitengeneza vyema tui la nazi, wapo wanaojua kutumia machicha lakini ninachotaka kusema kama nilivyosema hapo juu ni namna tu ya kupiga chakula ambacho kina kemikali zenye viamsha nyege.
Pia kuna aina ya mvinyo ambayo humfanya binti awe na hamu kubwa ya kufanya mapenzi. wapo wanaozungumzia divai na wapo wanaozungumzia amarula.

Uzito mkubwa si sahihi kwa afya na urembo wako


TUMEKUWA kila siku tukizungumzia masuala ya kuweka ngozi safi na sura bomba lakini mara zote huwa tunasahau kuzungumzia uzito ambao ama hakika ni kitu kibaya kuliko kitu chochote kile.
Uzito ni sawa na uvuitaji wa sigara ambao huleta matatizo makubwa kwa watu ambao wamo katika kilinge hicho.
wataalamu wa afya na urembo wanasema wazi kuwa kuwa mnene kunapunguza sibtu namna ya kujiweka sawa katika masuala mbalimba;li ya kijamii lakini pia unakuwa na muda mfupi sana wa kuishi duniani.
Wataalamu wanasema kwamba kuwa mzito kunapiunguza maisha yako kwa miaka mitatu anasema mtafiti Gary Whitlock kutoka Clinical Trial Service Unit ya chuo kikuu cha Oxford kilichopo nchini Uingereza.
Uzito huu ni ule unaokuwa mara tatu ya uzito ambao unhatakiwa mtu awe nao kutokana na urefu wake,umri na pia afya yake.
Ndio kusema kama mtu anakuwa na uzito mathalani paundi 150, mtu huyu anapunguza umir wake w akuishi hapa duniani kwa miaka 10.
Sasa kama unapunguza umri huo watu wako wanakupenda wtafanaya nini.
Kwa maelezo mengine ni kuwa uzito wa aina hii ni sawa na uviutaji wa sigareti ambapo pamkoja na kuchakaza ngozi pia hupunguza maisha ya mtu kwa miaka kumi.
Ndio kusema katika urembo pamoja na kupiga vita sigareti uzito wa kuchusha nao lazima upigwe vita.
Kwa wanawake wengi wa kiafrika wanadhani kuwa mnene ni kuonekana bomba, pamoja na kuwa mnene ni kutamu kwani unakuwa na nyama za kushikwa lakini ni vyema watu wakatambua kwamba uzito wa kuchusha yaani mara tatu ya ulke unaostahili kuwa nao ni hatari kubwa kwa maisha yako.
Onyo hili la wataalamu limefanywa baada ya uchunguzi kwa watu 894,576 waumde kwa wake katika tafiti 57 zilizofanywa.
ingawa tafiti hizi zilifanywa kwa watu wa Kaskazini mwa Marekani na Ulaya kwa watu wenye ujazo wa 25 (BMI) hata hapa nchini watu wanastahili kuangalia juzito wao.
Kwa taarifa yako uziuto wa kuchusha hule ta tatizo la figo, ini na aina kadha za kansa na pia hyuleta matatizo ya magonjwa ya moyo na kiharusi. Unene huleta mchosho mkubwa kwa moyo na pia kuleta mizania dhaifu ya rehemu na kusababisha shida katika mwenendo wa damu.
Wanaume wenye kiuno kikubwa huongeza hatihati ya kifo wakatiw nawake wenye mzunguko mkubwa huongeza hati hati ya kifo kwa asiulimia 78.

Wednesday, October 21, 2009

mambo yanayofaa kwa miguu minene


Ni kasheshe kubwa kuirembesha miguu mikubwa, lakini ni kweli kuwa unahitaji miguu yako hiyo kuwa na nafasi kubwa ya kuonyesha uzurui ulionao.Kipendezacho ni chako.Miguu mikubwa si mwisho wa fasheni unachotakiwa kujua ama hakika ni namna ya kuiweka vyema miguu yako na uonekane bomba.
Wapo watu ambao wamekuwa na miguu mikubw akutokana na sababu mbalimbali na pamoja na kuwa na miguu hiyo wka sababu ama z alishe au kutofanya mazoezi wewe kama binti au mke unataka nguo zako zisiwe na ubazazi na badala yake zionyeshe raslimali ulizonazo yaani uzuri wako.
Kama unataka kuweka miguu yako mikubwa katika hali bora ni lazima uanze kula lishe njema na pia kufanya mazoezi.
Kitu kingine kizuri kwa wewe mwenye miguu mikubwa au tuseme minene ni kuhakikisha kqamba unavaa nguo zinazofiti lakini nguo zinazobana sana si nzuri hata kidogo na zilizopana kabisa nazo mbaya kwani itaonekana mkiguu yako ni mikubwa sana kuliko unavyofikiri.
Wakati unavaa suruali mathalani, vaa ile ambayo ni pana ambayo haipigii tambo miguu yako.
na kama ni viatu lazima uwe unavijulia kwelikweli hata siku moja usivae buti na sketi ambayo inaonyesha miguu yao waziwazi.
nataka kusema hivi kuwa na miguu minene au tuseme mikubwa si tatizo, tatizo ni wewe namna unavyofanya mambo na namna unavyojiweka katika maizngira ya kupendeza na nguo zako za kupendeza ambazo hazibani wala hazipwai.
Na pia unaweza kwa namna nzuri kabisa kuachana na sketi na pensi nyanya ambazo zinakata laini ya miguu yako kama enka nakadhalika.
tengeneza staili ambayo utaonekana wa kawaida na u mrembo katika hilo.