Monday, September 28, 2009

Jinsi ya kuondoa kikwapa

Huhitaji fedha za kigeni kuondoa kikwapa .Ni juhudi ndogo tu ya kawaida ya usafi inaweza kukusaidia.Malimao na ndimu na vitu vyenye uwezo mkubwa wa kuondoa harufu na uchafu katika kwapa.
Wengi wamekuwa wakitumia sabuni, krimu na hata pafyumu za aina mbalimbali kwa ajili ya kuondoa uchafu wa kwenye kwapa lakini bila ya mafanikio yoyote.
Matumizi ya ndimu na limao yana matokeo mazuri kwamwili wako kama utatumia kikamilifu.
Unachotakiwa na kufutafuta limao au ndimu unaikata kisha unakamua. Chukua kitambaa weka maji maji ya limao na kisha anza kusugua taratibu kwapa lako.
Hakikisha unafanya hivyo wakati ukiwa umetoka kuoga. Pia unaweza kukata limao au ndimu bila ya kukamua na kuanza kusugua katika kwapa lako. Vitu hivyo vina nguvu za kuondoa uchafu katika kwapa.
Ni muhimu kusafisha kwapa kwani kwapa linapokuwa si safi hata unapovaa nguo ya wazi unakuwa huna uhuru wa kunyanyua mkono juu pindi inapokulazimu kufanya hivyo.
Kwapa ni sehemu muhimu sana ni lazima iangaliwe kwa namna ya pekee na uhakikishe unakuwa safi muda wote ili kuondoa harufu na muonekano mbaya katika kwapa.

Umuhimu wa manukato katika urembo wako

KARIBUNI wasomaji katika blogu hii ya urembo na utanashati.Leo naona tuzungumzie jinsi manukato yanavyoweza kuwa na manufaa katika urembo wako.
Ukitaka kuwa mrembo ni wazi kuwa unatakiwa kuuweka mwili wako katika hali nzuri ya kupendeza kuanzia mavazi, mitindo ya nywele.Ndio kusema kuna vikorombwezo kibao vinavyotakiwa ili kukufanya uwe mrembo zaidi.
Manukato nayo ni muhimu katika kunogesha urembo wako.Nadhani ulishawahi kusifiwa au kusifia mtu kutokana na manukao anayotumia na wengi wetu tumekuwa tukitumia aina za manukato ambazo tunaona zinatufaa zaidi.
Ni vizuri kuchagua aina ya manukato na njia nzuri ni kupulizia kigogo kwenye mkono wako ili uweze kujua harufu yake kama umependezwa nayo au laa. Usitumie manukato ya aina fulani kwa sababu fulani anatumia.
Jaribu kutafuta aina ya manukato uliyoyachagua kwani kuwa mnukato yana harufu kali na hili huleta taabu kidogo kwa baadhi ya watu unaokuwanao karibu.
Chagua manukato ambayo yana harufu iliyotulia na pia ukali wa manukato wakati mwingine husababisha kujipulizia kiasi kikubwa cha manukato hali ambayo huwa kero kwa wengine.
Jaribu kutumia manukato kiasi fulani kwani aina nyingine hudumu muda mrefu na unapojipulizia manukato ona unafanya hivyo kwa faida yako na sio kuhakikisha kuwa kila mtu anajua umetumia manukato ya aina fulani hapo ndiyo huleta shida kidogo kutokana na kutumia kiasi kikubwa cha manukato na hivyo kuleta shida kwa wengine.
Pia unashauriwa kutotumia manukato ili kuondoa harufu ya mwili kutokana na kutooga au kutokana na sababu nyingine hapo maana ya manukato hupotea. Manukato hupendeza iwapo yatapuliziwa wakati mwili na nguo zikiwa safi. Tumia aina ya manukato uipendayo ili kuweza kukuweka mrembo zaidi.

Namna ya kuondoa vipele na mafuta usoni

Ukiwa mwanaume au mwanamke upigaji sopusopu ni jambo la busara sana ili kukuweka mtanashati na mwenyekuvutia muda wote kwa kuondoa uchafu na pia kuondoa mafuta ambayo yana kawaida ya kutanda katika sura.
Kitendo hicho huitwa scrub.Husaidia kuondoa chunusi,vipele na makovu na pia inapunguza mafuta usoni.
Uso unapokuwa na mafuta sana na kuyaondoa kunasaidia kupunguza vitu vingi pamoja na vipele na hata mabaka yaliyosababishwa na vipele au chunusi.
Unaweza kutumia scrub ya kwa njia ya mikono kwa kila baada ya siku tatu, na scrub ya mashine baada ya mwezi mmoja.
Scrub ya mkono.Tafuta aina ya scrub inayokufaa kulingana na ngozi yako.safisha uso wako mpaka uhakikishe kuwa umetakata kisha chukua scrub na kuanza kusugua usoni taratibu kwa muda wa dakika tano kisha nawa uso na unaweza kupakalosheni au poda baada ya kunawa.
Scrub ya mvuke.Chesha maji Nawa uso kwa kutumia maji safi na uhakikishe kuwaumetakata.
Futa uso kwa kutumia taulo safi.
Paka scrub usoni na pia shingoni kama utapenda. Sugua uso kwa kutoa taka.Chukua taulo jifunike na kisha inamia beseni lenye maji ya moto.Baada ya dakika tano toka na subiri kwa muda wa dakika tano nyingine kisha nawa. Paka poda au losheni.
Pia unaweza kutembelea saluni za kisasa kwa ajili ya kuufanyia facial uso wako Pia unaweza kutafuta sabuni ya ukwaju na ukawa unanawa uso asubuhi na jioni hii huondoa upele, chunusi na mabaka usoni

Thursday, September 17, 2009

namna bora ya kutunza miguu



Sasa tuzungumzie juu ya utunzaji wa miguu. Miguu ni sehemu inayoangaliwa sana hasa kwa wanawake, kwani unapoamua kuvaa nguo fupi na huku miguu yako haiko katika hali ya kuvutia sina shaka utaanza kujishuku hata kabla ya kutoka nje.

Miguu ni sehemu ambayo inatakiwa kutunzwa kwa kipekee kama ilivyo sehemu nyingine kama uso. Wengi tumekuwa tukipendezesha nyuso zetu na kusahau kbisa habari za miguu.

Haijlishi miguu yako ni miembamba au minene iwapo utaitunza vizuri sina shaka kuwa utavutia kwa nguo yoyote utakayoivaa.

Kuna njia nyingi za kutunza miguu na unaweza kutunza miguu yako hata kama huna fedha za kununulia vikorokoro vinavyotakiwa.

Unaweza kuchukua beseni na kuweka maji ya uvuguvugu yenye povu la sabuni maalum ya kuoshea miguu kisha loweka miguu na iache kwenye maji kwa muda wa robo saa hivi.

Chukua aina ya scrub uliyoichagua kwa ajili ya miguu yako paa na ikikauka anza kusugua miguu yako na hadi kwenye vidole na unyayo.

Kisha jisafishe kwa maji ya uvuguvugu.

Baadhi ya vitu unavyoweza kutumia ili ku kutengeneza miguu yako ni pamoja na foot file, Therapysa virgin vie salt scrub, Pedicure iliyotengenezwa kwa OPI Refresh Cooling ffot Gel, Innoxa cool na Calm liquid talc na Feet first reviving Foot Soak.

Bidhaa hizi unaweza kuzipata kwenye duka kubwa la vipodozi na pia utpata maelezo jisi ya kutumia

Pia unaweza kutembelea baadhi ya saluni ambazo zinatoa huduma hiyo jitahidi hata mara moja kwa mwezi kuhakikisha miguu yako inapata huduma nzuri ili iwe ya kuvutia.

Kwa wale ambao miguu yao ni makovu au madoadoa wajaribu kutumia scrub na kama hawatafanikiwa kuondoa tatizo hilo basi wanashauriwa ktumia cream na sabuni zenye mchanganyiko wa ukwaju kwani zinasaidia sana kuondoa madoa.

Pia unaweza kuchukua mkwaju ukaloweka kwenye maji ukishalainika changanya mchanganyiko huko na asali kasha paka.

Husaidia kuondoa madao na hata kwa wale wenye ngozi za mafuta na chunusi sugu mafuta yatakauka na chunusi hazitatoka tena.

Namna ya kuhami ngozi laini inayozunguka jicho


Ngozi yako inayozunguka jicho ni sehemu muhimu sana kwani ina ulaini na inahitaji uangalifu mkubwa.
Sehemu hii ya ngozi ni nyembamba mno na inaweza kupata madhara na kitu kidogo kabisa ili hali inaweza kuzeeka mapema kabisa kabla ya muda wake.
Ndio kusema lazima ufanye mambo fulani kila siku, mchana na usiku, ili kuhakikisha kwamba sehemu hii inabaki vyema kama inavyostahili.
Swala la kwanza muhimu ni kwamba ni lazima uoshe vitu vyote ulivyotumia kuremba jicho lako kwa kutumia visafishaji ambavyo si vikali.
Bidhaa nyingi zinazotengenezwa kuondoa make up katika jicho zimetengenezwa katika mazingira ya kuhakikisha kwamba ngozi inabaki hai na isiyokuwa na matatizo.
Moja ya kisafishio kizuri amnacho kina uasili ni kile cha witch hazel.Bidhaa hii inafanyakazi ya kuondoa make up huku eneo likiachwa katika hali yake.
Inatakiwa kila asubuhi unapoamka asubuhi ni vyema ukaanza na eye gel au krimu yenye unyevunyevu na unapoenda kulala wakati wa usiku.
Kwa kuwa umri unavyozidi kuongezeka ngozi huacha kujirejesha inavyotakiwa na huondoa ule ulaini wake iliokuwa nao kwanza kuhakikisha kwamba eneo hilo lina unyenyevu husaidia kuweka ngozi ile katika hali bora zaidi.
Ni vyema ukahakikisha kwamba moisturizers unayotumia ina SPF ili kuhakikisha kwamba ngozi inayozunguka jicho inahamiwa vyema dhidi ya mikunjo inayosababishwa na miale ya jua.
Njia nzuri pia ya kupunguza uvimbe wa macho ni kuweka mask kuzunguka jicho.
Pia unaweza kumasaji eneo hili ili kuondoa sumu ambayo imjijenga katika mfumo wa liymph.
Watu wengine huhifadhi eye cream kwenye friji na kutumia kumasaji eneo hilo ili kuondoa mauamivu yanayokuwepo.
Tatizo la mikunjo katika ngozi inaweza kudhibitiwa kw akutumia bidhaa za urembo zenye asidi ya glycolic ambayo pia hujulikana kama alpha hydroxy acid au AHA.
Moja ya bidhaa bora zaidi zinazosaidia kuondoa mikunjo ya uzee kuzunguka jicho ni Olay. kuna bidhaa nyingi bora ambazo zinaweza kabisa kuondoa miukunjo .
Kuna njia pia za asilia mbazo zinaweza kusaidia kuweka sawa ngozi inayozunguka jicho kama vipande vya matango.
Pia unaweza kutumia mafuta olive oil kuzunguka macho yako kila siku na utaona matokeo yake yatakavyokuwa bora.

Monday, September 14, 2009

uondoaji chunusi kwa njia za kiasili


Ukitaka kuondoa chunusi usoni na kusafisha uso usiwena madoa kwa kiasili, njia zifuatazo zaweza sana kusaidia.
Tafuta ukwaju loweka katika maji ukishalainikachanganya na asali, paka usoni.
Ni dawa nzuri sana na utaona ngozi yako inabadilikakwa kipindi kifupi.
Kama utashindwa kupata vitu hivyo tafuta sabuni pamojana krimu yenye mchanganyiko wa asali na ukwaju.
Sabuni hiyo iko katika boksi kubwa na kwa ndani inakigunia ambacho kinasaidia kusaficha uso, usinunue sabuni ya ukwaju na asali ambayo haijafungwa kwenye kitambaa kigumu chenye rangi ya kahawia itakuwa ni feki na haitakusaidia.
Kama unataka kupunguza tumbo au mwili kwa ujumla.Asubuhi kunywa chai nzito, mchana kula chakula kilichokamilika.
Ila usiku kula matunda tu ili uweze kuupa mwili nafasi ya kujitengeneza na hasa kupunguza mfuta yaliyozidi mwilini.
Uwe unakula wakati unasikia njaa tu unapokula bila yakusikia njaa unakuwa unarundika tu chakula mwilini na baadaye chakula hicho hubadilika na kuwa mafuta ambayo
hutengeneza manyama uzembe.
Ukishindwa hivyo nenda kwa daktari iliakupe masharti ya vyakula na uweze kupunguza mwili

Jamani hebu hurumieni nguo zenu, zitunzeni


Watu hutumia mamilioni kama si maelfu ya fedha zao kwa ajili ya kuhakikisha kwamba wanakuwa bomba na wenye kuvutia. Lakini ni kawaida mno kuona watu hao hao wakitupa fedha hizo kwa kuzivuruga nguo zao na kuziweka pasipo heshima kiasi ya kwamba huchakaa haraka au huharibika kwa muda mfupi sana.

Wengi wetu ambao tuna haki ya kujiita watanashati tuna matatizo makubwa sana ya utunzaji wa nguo zetu na wakati mwingine tunasahau kwamba nguo hizo ni raslimali zetu ambazo zikiharibika na sisi vile vile tunaharibika.

Mathalani mtu ananunua nguo kwa paundi 4000, fedha nyingi kabisa, lakini mtu huyu ambaye alitakiwa kuheshimu nguo zake unaweza kuingia chumbani mwake ukazikuta zimetupwa tu holela kitandanim, kwenye kochi na wakati mwingine hata bsakafuni.

Wewe mtu anavua suti na kuitupa, mtu anavua sidiria na kuitupa yaani mambo yote hata hayaeleweki.

Lakini nataka kusema hivi unapokuwa unabadilisha nguo kumbuka kuzihifadhi na kuzitunza kwani hiyo ni raslimali zako mwenyewe.

Kutokana na hali hiyo nataka kukueleza kuwa nguo ziku zote zinatakiwa kuwekwa kwa urefu wake ili zirejee katika hadhi yake ya kawaida.

Ni vyema kwelikweli na nasisitiza kuweka nguo zako kwa kuzitundika ili zirejee katika ule uzuri wake wa dukani na katika matenegnezo.

Ni vyema kama kabati lako halina nafasi ya kuweka vining'inizo ukaviweka kwani ni vya maana sana hsa vile vilivyotengenezwa kwa mbao.

Na wakati mwingine tumia vishikizo ambavyo vinasimamiwa pia na vitu vngine. Ninachotaka kusema hatakama ni sketi iweke katika nafasi yake inayostahili.Vivyo hivyo kwa jaketi na suruali na hata mashati.

Pamoja na kuweka nguo yaani kuzitundika ili kupata uhalisi wake ni vyema pia kuwa na mpango katika kabati lako si tu kujifanyia mambo kama mwendawazimu.Manake kama hukuwa na mpango itakuchukua siku nzima kujua ni wapi umeweka brazia au nguo yako ya ndani.

Ni lazima siku moja uamue kufanya ratibu ya kabati ili liwe na maana kubwa kwako na kukuwezesha kufanya maamuzi ya kasi wakati wa kuchagua nguo za kuvaa ziwe za ndani au nje.

Naomba usiruhusu kwa namna yoyote ile uwekaji wa mifuko ya nailoni kwani hutunza hewa ya unyevu na hii huleta uvundo katika nguo.

Pia kufanya mambo yako yawe bomba tafadhali fanya mambo mawili. Moja hakikisha kwamba nguo za zamani unazitoa ambazo zimemalizika muda wake wa fasheni.

Na maana kubwa sana ni kuwa upangaji husaidia pia kukuwezesha kufanya mambo ambayo pengine huyapati kwa uzuri kuwa na nafasi ya kuona.

Utunzaji wa nguo hauko tu katika kuziweka vyema bali hata wakati wa kufua,Angalia kwa makini maelezo ya nguo zako, maji yanayostahili kutumika joto na pia aina ya sabuni. Na ukishamaliza basi zinyooshe kama zinavyotakiwa.

katika masuala haya ni pamoja na viatu kuangaliwa, kusafishwa na pia kutunzwa kwa mujibu wa maelekezo ikiwemo ya utiaji wa kiwi.

Wednesday, September 9, 2009

Umaridadi wa kupaka rangi kucha


Ili uwe na kucha maridadi masuala ya kuzisafi na kuziweka rangi ni muhimu ama sivyo? na kwa kawaida kucha zilizo safi ndizo hasa zinazokubali polishi yaani rangi au sivyo?

Na ama hakika kucha zilizo safi ndizo hasa zinazotengenezwa na kuwekwa sopusopu.

Ni vyema kutambua kwamba wakati wa kupaka rangi tumia mipako michache kwa kila mpako na kila mpako uachie ukauke kabla ya kuanza mpako mwingine.

Na ile ya mwisho inatakiwa kuwa bomba zaidi kwa kuwa ndio hasa itakayokuwa inatunza matabaka mengine yote.

Utengenezaji mzuri wa kucha si lazima uwe wa kwenda katika mapumziko au kuonyesha mtu ni kitu ambacho kinafaa kufanywa ili uwe mrembo kila mahali.

Kuna raha ya kujisikia katika rangi mpya katika mwaka mzima na hasa kama uchaguzi wako wa rangi za kupaka ni bomba.

Moja rangi ya pinki ama nyekundu inakupa nafasi ya kuwa funny . Unaweza kujipaka rangi mwenyewe au kuwambia mtu akupake rangi.Kuna hatua kadhaa ambazo unatakiwa kuzifanya kabla ya kupaka rangi kucha zako.

Hatua ya kwanza ni kuondoa rangi zote za awali.kwa kufanya hivyo rangi mpya itakuwa ina uwezo wa kushika katika kucha.

Pia kunasaidia rangi yako mpya isitibuliwe na rangi ya zamani kwa namna yoyote ile.

Unaweza kuondoa rangi ya zamani kwa kutumia dawa inayopatikana katika maduka ya dawa na hata yale ya vipodozi na pamba hufanya vyema kartika kuondoa rangi za kucha kwa kutumia Nail polish remover.
kazi ya pili ni kutafuta rangi inayokupendeza. unaweza kutumia rangi yoyote kwa sababu mara nyingi viatu vinazuia kuonekana kwa kucha zako la kama unahitaji rangi fulani kwa sababu miguu yako i wazi ni vyema sana.

Tazama kwamba vipaka rangi vyenyewe ni vipya kwani vilivyozeeka huleta tatizo kidogo.mara nyingi vipaka rangi vilivyokaa miaka miwili havifai tena kutumika.

Anza kupaka baada ya kubainisha kwamba unaweza kutenganisha kidole kwa kidole ili usipake kila mahali hasa kama brashi husika ni pana kidogo.

Anza katikati kwa kuanzia nyuma kupeleka mbele kisha nenda pembeni na pembeni.Na baada ya kukauka unaweza kuongeza tabaka jingine tena na tena.

Kisha paka ile ya mwisho ambayo ndiyo italinda rangi yenyewe yaani top coat . top coat husaidia sana kuweka rangi kwa muda mrefu. Top coat ni polishi isiyokuwa na rangi na kama unataka kuweka stika iweke mapema kabla ya kuweka top coat.
rangi nzuri na zilizotulia zinakufanya uwe na sababu ya kujivalia sandals zako nzuri au viatu vya wazi

Monday, September 7, 2009

Viatu visivyofaa vitakuletea ugonjwa







Wanawake wana kazi kubwa katika kuhakikisha wanaonekana wapo warembo na wana urefu unaotakiwa. Katika hali hiyo inaaminika kuwa katika wanawake wanne kati ya kumi wananunua viatu visivyowafaa wala kuwatosha.
Kura ya maoni iliyohusisha watu 2000 iliyofanywa na The Society of Chiropodists and Podiatrists imeonyesha kuwa asilimia 37 huvaa viatu vinavyowapa shida ili mradi tu wawe katika fasheni.
Asilimia 80 ya wanawake wanasema kwamba hali hiyo huwafanya wapate matatizo ya miguu kama kuota vigimbi , ukuaji wa kucha usiostahili lakini hawatafuti hata msaada wa daktari.
Lorraine Jones, kutoka Society of Chiropodists and Podiatrists, anasema kwamba hili tatizo la kutaka fasheni linaharibu afya za wanawake.
Inashauriwa kwamba mwanamke avae kiatu ambacho hakina urefu wa zaidi ya sentimeta nne na pia kina uduara kwa mbele.
Ni vyema mwanamke akaelewa kwamba kama anajisikia maumivu basi mambo si shwari hata kidogo.

Sunday, September 6, 2009

Mikato ya nywele inafaa kuzingatia kichwa











Hakuna kitu kinachofurahisha kama nywele za mwanamke. Nywele za mwanamke zinapowekwa sawa na uso wake, humfanya awe na mng'ao usiokuwa wa kawaida.
Nywele za mwanamke zinaheshimika zinathaminika na ama hakika ni hazina moja ya maana kwa mwanamke iwe zimekaangwa au zimewekwa tu kama vile mchemsho.
Nywele na staili zake hazijabadilika sana ingawa zamani nywele zilikuwa zinawekwa vitu vingi katika mizungusho ya kawaida ya kuremba na wakati mwingine kuachwa tu zikijiotea na wengine wakitumia muda mwingi kuzisuka.
Ni vyema kama mwanamke unataka kupendeza kichwani kufika kwa wataalamu wa nywele ambao watazitengeneza au kukupa ushauri kutokana na kichwa chako na si vingine.
Ni kutokana na hali hiyo lkeo tunakuletea picha mbalimbali za watu na miondoko yao kichwani kwa lengo la kukuonyesha kwamba unachosuka kichwani inafaa kifanane na kichwa chako.
Si misuko tu bali hata utengenezaji wa huria wa kutumia dawa au hata dawa za asilimi ni lazima izingatiwe ukubwa wa kichwa na namna ambavyo ungelipenda wewe uonekane.
Zamani misuko ilikuwa ya kuchekesha zaidi na matumizi ya kofia yalimaliza utata uliopo kichwani kwa wakati unapoangaliwa kwa makini.
Nataka kukuambia kwamba nywele nyingi hutengenezwa kwa kuangalia unataka kumvutia nani na kwanini.

Chumvi,sukari nyingi huzeesha ngozi


Shosti niwaambieni kuwa matumizi makubwa ya chumvi au sukari ni hatari na sumu kubwa katika ngozi zetu kwani husababisha ngozi kuwa na makunyanzi kabla ya umri.

Kawaida makunyanzi hutokea unapokaribia kuimaliza miaka ya 40.Watu ambao ngozi zao zimeathiriwa na matumizi makubwa ya sukari na chumvi wanashauriwa kupunguza matumizi yavitu hivyo kwa kula mboga za majani na matunda kwa wingi ili kuweza kuondoa sumu ambayo imejengekamwilini na pia kunywa maji mengi.

Wanasayansi wanasema kuwa, watu wanaotaka kutunza ngozi zao kutotumia sukari kwa wingi kwani sukari huchangia kuzeesha ngozi. Sukari nyingi hufanya misuli ya protini katika ngozi kujikusanya pamoja na kusababisha kutoweka kwa mnyunyuriko unaotakiwa.

Ili ngozi iwe laini ni yema ukanywa maji mengi, maji husaidia kulainisha miili yetu kwani mwili unapokuwa hauna maji ya kutosha unakuwa mkavu na ngozi haipendezi hata kama unatumia vipodozi vya aina mbalimbali na vya gharama. Ni bora kuulisha na kuunywesha mwili wako ili ngozi ijitengeneze yenyewe.

Wednesday, September 2, 2009

Namna yakujiweka fiti kwa mwanamke


Katika kujiweka fiti au tuseme kujiweka sawa kwa ajili ya kuonekana mrembo ni kazi ambayo inahitaji muda na uvumilivu vinginevyo unaweza kuwa sawa na chizi yoyote aliyejiwekea si tu maleba bali na mwili usiotamanika.

Na kwa mwanamke ambaye ana mji wake, watoto , familia na kazi inayohitaji ukakamavu mkubwa huku akitakiwa kuonekana bomba namchangamfu ni dhahiri kuwa la ziada lazima lifanyike vinginevyo mahali fulani utapwaya.unaweza kupwaya ofisini, ukaonekana huna maana , unaweza kupwaya nyumbani mtoto mkubwa akashindwa kukuangalia mara mbili na unaweza kupwaya mtaani watu wakajiuliza hee mama fulani vipi mbona usafi unamshinda?ndio kusema katika hili unahitaji mwanamke kuwa makini sana.

Inavyoonekana wanawake wengi wanapokuwa katika mtawanyiko wa mambo hujisahau kabisa na mara nyingi husahau kabisa kuwa wanahitaji kula nakufanya vitu fulani ili kujiweka fiti.Kimsingi wanawake wote wawe wanachapa kazi kama wazimu, wawe na familia, wawe na mtoto mkubwa wanatakiwa kujiweka safi na sawa muda wote pamoja na majukumu yao yaliyotawanyika.

1) suiku zote hakikisha una tunda wakati wa kifungua kinywa chako. Hiiinasaidia kuondoa sumu katika mwili wako na kusaidia kuondoa uchafuuliojiweka kwa namna inavyostahili.

2) Kunyw amaji ya kutosha , punguza chai na kahawa kufikia angalauvikombe viwiuli kwa siku na muda uliobaki kunywa vinywaji ambavyo nivya mizizi kama jasmine, chamoile tea. Vinywaji hivi katika mfumoi wajuisi ni dawa tosha kwa ngozi yako na ili ionekane ya ujana muda wotena isiwe kavu.

3) Huku umri wako ukiwa unapanda,punguza vyakula vya nafaka na kulazaidi matunda na mbogamboga ili kupunguza uzito.

4) hakikisha unatembea vya kutosha na kujinyoosha ili uwe na mwili wakuvutia, mwembamba na wenye nguvu za kutosha na wa ujana.
5) Punguza uvutaji sigara na pombe kwani ni vitu viwili vinavyozeeshangozi kwa kasi.

6) Ongeza vyakula vya samaki katika chakula chako au aina yake

7) Uwe unakula na mizizi inayokabiliana na uzee kama tulsi, amla, ashwagandha

8) Jipatie vitamu vya asili kama asali na raisins.

9) Kula vyakula vyako unavyopenda vya hovyo angalau mara moja kwa wiki

10) Kujisikia vyema ni namna bora za kukufanya uwe mwanamke bomba naanayevutia muda wote.

NB:Kujisikia vyema huku ni kujipenda mwenyewe kama hujipendi huwezi kuvutia na kama unaridhika kwa sababu ya kuridhika una tatizo kwelikweli.